RC Akiapishwa

Dk. John Pombe Magufuli akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha ,Mhe. Mrisho Gambo.

Ziara ya Waziri Mkuu wa Tanzania

Mhe. Mrisho Gambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa Ofisini kwake, Jijini Arusha.

JPM ,Mrisho Gambo Picha ya Pamoja

Dk. John Pombe Magufuli akipiga picha ya pamoja na mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.

Samia Suluhu Hassan akiwasili Jijini Arusha

Mkuu wa Mkoa Arusha, Mhe Mrisho Gambo Akimpokea Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Picha ya Pamoja

Mhe. Mrisho Gambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa.

Showing posts with label Utalii. Show all posts
Showing posts with label Utalii. Show all posts

Wednesday, October 10, 2018

TAIFA LISILO NA UTAMADUNI NI TAIFA LILILOKUFA

Katibu mkuu wa wizara ya habari,Utamaduni,sanaa na michezo, Suzan Mlawi amesema,Taifa lisilo na utamaduni ni taifa linalokufa na kutoa kizazi kisichoweza kuenzi na kuthamini mila na desturi zao.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua tamasha la Urithi wa Utamaduni katika mkoa wa Arusha lililoanza Octoba 8, 2018 hadi Octoba 13 katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid.

“Nimefarijika kuona tamasha hili litakuwa linafanyika kila mwaka, kwani litatoa nafasi kubwa sana kwa watanzania kujifunza tamaduni mbalimbali na pia litaenzi mila na desturi zetu kwa kiasi kikubwa”,alisema.

Amesema kupitia tamasha hili anategemea kuona ukuaji wa uchumi kwani bidhaa nyingi za asili zitapata masoko,kufufua mila na desturi zilizokufa kwa vijana wa sasa.
 Mwenyekiti wa kamati kuu ya maandalizi  Pro.Audax Mabula, amesema tamasha hili lilizinduliwa mnamo Septemba 15,2018 na makamu wa Rais mheshimiwa Samia Suluhu Hasan mjini Dodoma na kuendelea  Zanzibar, Dar es Salaam na sasa lipo mkoani Arusha.

Amesema lengo kubwa la tamasha hili ni kuenzi mila na malikale za Kitanzania kwani ni kwa mda mrefu sasa  utamaduni wa watalii ndio umekuwa ukipewa kipaombele zaidi kuliko huu utalii wa utamaduni.

Kupitia tamasha hili la urithi wa utamaduni itasaidia kuutambulisha zaidi urithi wa utamaduni katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.

 Nae katibu tawala wa mkoa wa Richard Kwitega amesema tamasha hili kwa mkoa wa Arusha litasaidia kwa kiasi kikubwa kudumisha mila na desturi za makabila ya mkoa huu na pia kuwakutanisha makabila mbalimbali na kuweza kujifunza tamaduni zetu.

Tamasha hili la urithi wa utamaduni lilizinduliwa kwa mala ya kwanza nchini jijini Dodoma na litakuwa likifanyika kila mwaka kwa mwezi mzima wa Septemba katika mikoa mbalimbali na kwa Mkoa wa Arusha linafanyika pia katika wilaya ya Karatu.






Friday, September 28, 2018

VIONGOZI WA MILA WATAKIWA KIRITHISHA MILA NA DESTURI ZAO.

Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dokta. Harrison Mwakyembe akiongozana na viongozi mbalimbali wa mila wa kimaasai na wacheza ngoma, alipohudhuria mkutana wa baraza la viongozi wa koo na rika,jijini Arusha.


Dokta. Mwakyembe akipokea baraka kutoka kwa viongozi wa kimila la kimaasai katika mkutano wao na kiongozi huyo.


Waziri  Dokta. Mwakyembe akivalishwa zawadi ya mgololi kama ishara yakusimikwa kuwa mmoja wa wazee wa kabila hilo la Kimaasai,Arusha.


Waziri Mwakyembe akipokea fimbo kutoka kwa kiongozi wa mila kama ishara ya kuwa mmoja wao kwenye kabila la Maasai,Arusha.




Friday, April 27, 2018

KATIBU TAWALA AKUTANA NA WAJUMBE KUTOKA BENKI YA DUNIA

Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega, akiwa na wajumbe kutoka Benki ya Dunia ofisini kwake pamoja na wataalamu kutoka katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Arusha.


Kiongozi wa ujumbe kutoka Benki ya Dunia Bwana Nicholas Soikan (mwenye suti ya blue) akiandika maelezo yaliyokuwa yanatolewa na wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa (Hawapo pichani),katika ofisi ya katibu tawala,Arusha.


Katibu Tawala Bwana Richard Kwitega,akiongoza kikao kilichowakutanisha ujumbe kutoka Benki ya Dunia na wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Arusha.



Taarifa ya Mkuu wa Mkoa Arusha katika kipindi cha TUNATEKELEZA.

Monday, April 9, 2018

ZIARA YA RAIS MAGUFULI-ARUSHA

Rais Magufuli akihutubia wananchi wa Arusha katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid katika sherehe za uzinduzi na ufunguaji wa kituo cha utalii cha polisi na nyumba za makazi ya polisi,jijini Arusha.

Saturday, April 7, 2018

Rais Magufuli Afungua Kituo Cha Utalii Cha Polisi

Rais John Pombe Magufuli akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa kituo cha polisi cha Utalii,kulia kwake ni Ispecta Simon Sirro (Mkuu wa Polisi) na kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya ndani Mwigulu Nchemba,jijini Arusha.


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, ametoa Bilioni 10 kwa ajiri ya ujenzi wa nyumba za polisi wa vyeo vya chini nchi nzima.
Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na jeshi la polisi la mkoa wa Arusha katika sherehe za kuzindua  ofisi ya kidiplomasia ya utalii,Nyumba za makazi ya polisi na vituo 2 vya polisi wilayani Arusha.
Amesema kutokana na juhudi zilizofanywa na mkoa wa Arusha wa kujenga nyumba za polisi 31 baada ya nyumba 13 kuungua na moto mnamo Septemba 2017 na kusababisha familia 14 kukosa makazi.
Amewataka wakuu wa Mikoa wengine nchini kuiga mfano huo wa kujenga nyumba za polisi kwa  kuwashirikisha wadau mbalimbali kwani zilizoungua ni 13 na zimejengwa 31 zaidi ya zilizoungua.
Hata hivyo amewashauri pia wabunge watumie kiasi cha fedha cha mfuko wa jimbo katika kusaidia kujenga nyumba za polisi katika majimbo yao badala ya kuwaachia wakuu wa mikoa peke yao.

Rais Magufuli akizindua nyumba za makazi ya polisi ya Naura,akiwa na waziri Mwigulu Nchemba na Ispecta Simon Sirro, jijini Arusha.

Aidha, Magufuli ametoa ajira 1500 ya wahitimu wa jeshi la kujenga Taifa(JKT) kuajiriwa katika jeshi la polisi, ili kuongeza nguvu zaidi katika maeneo mbalimbali ya nchi katika kulinda usalama.
Amelitaka jeshi la polisi kuendelea kuchapa kazi kwa bidii kwani amefurahishwa na maonyesha yaliyoonyeshwa katika sherehe hizo ambayo yametoa picha nzuri kwa nchi kuwa jeshi la polisi lipo imara na yeye ataendelea kuwaunga mkono kwa kila watachoamua kufanya.
Magufuri amelitaka jeshi la polisi nchini kurekebisha mapungufu madogo madogo yaliyojitokeza katika jesho hilo yakiwepo ya rushwa na uonevu kwa wananchi ambayo yamekuwa yakichafua jina la jesho hilo kwani yanafanywa na baadhi ya polisi.

Rais John Pombe Magufuli akiteta jambo na mkuu wa Polisi Ispecta Simon Sirro katika sherehe ya uzinduzi wa kituo cha utalii cha polisi,jijini Arusha.

Akisoma taarifa fupi ya ujenzi Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Simon Sirro amesema ujenzi wa kituo cha polisi cha kidiplomasi kimegharimu kiasi cha shilingi milioni 193 ambapo ni michango kutoka kwa wadau na serikali.
Aidha, katika ujenzi wa kituo cha polisi cha Murieti kimegharimu kiasi cha milioni 260 na ujenzi wa nyumba za polisi 31 zimegharimu kiasi cha milioni 550 ambapo milioni 250 zimetoka serikalini,milioni 50 zimetolewa na polisi na wadau mbalimbali wamechangia kiasi cha milioni 250.
Amesema jeshi la polisi nchini limeendelea kulinda usalama wa raia na mali zao na hivyo kupelekea kupunguza matukio ya uharifu kwa kiasi kikubwa na hata pia kudhibiti ajari za barabara kwa kiwango kikubwa.

Kikosi cha kuzuia uwarifu cha jijini Arusha kikionyesha moja ya maonyesho yake mbele ya Rais Magufuli (hayupo pichani)  katika sherehe za uzinduzi wa nyumba za makazi ya polisi, Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amemshukuru Rais kwa juhudi zake alizozifanya katika kuleta maendeleo kwa mkoa wa Arusha katika nyanja mbalimbali hasa upatikanaji wa maji safi, ujenzi wa barabara,uboreshaji wa huduma za afya na kuboresha elimu kwa ujumla.
Aidha, amesema mkoa wa Arusha umeendelea kuleta maboresho zaidi katika sekta ya elimu kwa kuandaa utaratibu wa kutunga mtihani mmoja kwa shule zote za mkoa wa Arusha,ambapo awali kila shule ilikuwa inaanda mitihani yake.
Rais Magufuli yupo mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku 2 ambapo alitokea mkoani Manyara huko  alikabidhiwa ukuta wa machimbo ya Mirerani na sasa anaendelea na ziara  yake mkoani Arusha.


Kikosi cha polisi chakuzuia ghasia(FFU) kikionyesha namna yakuzuia maandamao mbele ya Rais Magufuli (hayupo pichani) katika sherehe za uzinduzi wa kituo cha polisi  cha utalii,Arusha.


Monday, March 12, 2018

Wajasiliamali wa Vinyago Kukuza Soko

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dokta Harrison Mwakyembe,akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro akimwelezea namna soko la vinyago linavyofanya kazi, pembeni ni Mwenyekiti wa soko hilo Elias Rajabu.

Waziri wa habari, utamaduni,sanaa na michezo Dokta Harrison Mwakyembe amewataka wajasiliamali wa vinyago kutafuta zaidi soko la bidhaa zao za asili ili kukuza kipato na kuendelea kutangaza utalii wa utamaduni.

Ameyasema hayo alipokuwa akuzunguza na wajasilimali wautalii wa utamaduni katika soko la Masai,jiji Arusha.Amesema bidhaa za utalii wa utamaduni ni nembo tosha yakutangaza nchi yetu.

“Ni kweli kuna Changamoto katika ujasiliamali huu wa utalii wa utamaduni hususani kwenye tozo mbalimbali mnazotozwa na mamlaka husua.”

Serikali ipo tayari kwenye mchakato wakutatua Changamoto hii ya tozo na kuona ni namna gani soko la vinyago nchini Tanzania linakuwa na kujulikana zaidi kimataifa, kuliko kwa sasa soko kuu linajulikana lipo jijini Nairobi wakati wazalishaji wakubwa ni  watanzania.

Dokta Mwakyembe alikuwa kwenye ziara ya siku 3 Mkoani Arusha,ambapo ameweza kufungua redio mpya ya kijamii (TBC FM),aliweza kutembelea kituo cha redio cha Sunrise,alifungua mkutano wa maafisa habari na mawasilino serikali,ameweza kukutana na wadau wa utamaduni,sanaa na michezo na ameweza kutembelea soko la vinyago la jijini Arusha.

Waziri Mwakyembe akizungumza na baadhi ya watalii waliofika katika soko la vinyago,jijini Arusha.


Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dokta Harrison Mwakyembe akitazama moja ya bidhaa zinazopatikana katika soko la vinyago jijini Arusha.


Waziri wa Habari ,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dokta Harrison Mwakyembe, akipokea zawadi ya kikombe kilichotengenezwa kwa shanga kwa mmoja wa wajasiliamali wa soko la vinyago jijini Arusha.


Monday, April 10, 2017

Wafanyabiashara Arusha wafarijika na maelekezo ya RC Gambo


Saturday, March 25, 2017

Kamati iliyokuwa ikishughulikia mgogoro wa pori tengefu Loliondo imemaliza kazi yake.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha , Mrisho Gambo katikati mwenye shati jeusi na nyeupe akiwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati iliyoundwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa eneo la kijiji cha Ololosokwan kilichopo Wilayani Ngorongoro ambapo hiyo ipo kwaajili ya kuingilia maeneo muhimu yanayofaa kwaajili ya uwekezaji,wanyama na binadamu. 


WANANCHI wa Kata Saba Wilayani Ngorongoro ambao wamekubaliana kwa pamoja kwenye mapendekezo yao juu ya kufikia muafaka wa mgogoro wa eneo la Pori Tengefu la Loliondo lenye kilomita 1,500 za mraba
wamesema kuwa endapo maoni yao yatakubaliwa na Waziri Mkuu,Kassim
Majaliwa watakuwa na nidhamu juu ya matumizi bora ya ardhi.
Wakizungumza jana Wilayani hapo wakati wa kikao cha pamoja juu ya
kukubaliana kama eneo hilo la Pori Tengefu Loliondo liwe chini ya
Jumuiya za Hifadhi ya Wanyamapori  za Jamii (WMA) au Pori Tengefu (GCA) kwaajili ya wanyama pekee ,wananchi hao walipendekeza kwa pamoja kuwa eneo hilo ni vyema likawa WMA ili jamii iweze kunufaika na maliasili zilizopo.
Wakizungumza jana mbele ya Kamati ya Utatuzi wa Mgogoro huo wa matumzi ya Ardhi ya Pori Tengefu la Loliondo, ambayo inaongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo wanachi hao walisema ni bora Pori hilo likawa chini ya WMA ili vijiji vinavyozunguuka kata hizo viweze kunufaika na mapato yanayotokana na utalii.

Lakini wengine wakiongozwa na Yanick Ndoinyo walionyesha hofu ya kuwa
na WMA kwa madai kuwa mapato ya kijiji kimoja hivi sasa yatakwenda
kwavijiji vyote vilivyopo kwenye kata saba zilizohusishwa na mgogoro
huo.


“Yani hapa tunatatua mgogoro lakini tunatengeneza mgogoro mwingine
maana ni lazima vijiji vipimwe na tukubaliane kuwa wamoja na kugawana
fedha hofu yangu ni kuwa je vile vijiji vinavyopata hela hapo awali na
hazijulikani zinakwenda wapi vitakubali”.


Alisema ngoja tuone maana tuliyokubali ni sisi kutoa mapendekezo haya
na endapo yatakubaliwa na Waziri Mkuu, Majaliwa hii itatutafuna
wenyewe kwa wenyewe maana hii ngoma bado nzito lakini tunamshukuru Rc Gambo kwa uamuzi huu ila ni lazima tukubaliane juu ya suala hili.
Lakini hoja za kuwa WMA zilipingwa kitaalam na  wahifadhi kutoka
Hifadhi mbalimbali za Taifa,ambapo Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori,
Profesa ,Alexander Songorwa alisema kuwa haiezekani mtoto akawa na
mama wawili huku akimaanisha kuwa sheria za wanyamapori na sheria ya
WMA zinakinzana.


“Ili pori hili liweze kuendelea ni lazima kuhakikisha Ikolojia hii
inahifadhiwa kwaajili ya kulisha Hifadhi ya Serengeti pamoja na eneo
hilo la Pori Tengefu kuwa la mazalia ya wanyama hivyo eneo hilo endapo
litaenda WMA hifadhi hii ya Serengeti itakufa”.
Alisema lakini haya ni mapendekezo tu yanaweza yakakubaliwa au la
hivyo kila mtu amesema analitaka kwaajili gani na mwisho wa siku
Waziri Mkuu,Majaliwa atapokea mapendekezo hayo na kasha kutolewa
maamuzi.


Kamati hiyo iiliyoongozwa na Rc Gambo ilikuwa Wilayani Ngorongoro
tangu Machi 15 hadi Machi 21 mwaka huu huku ikikumbana na manadamano ya mara kwa mara kwa wananchi lakini pia wajumbe hao wa kamati walaifanya kazi usiku kucha kushughulikia mgogoro huo kwa kukusanya maoni ya wafugaji,wahifadhi pamoja na wataalam wa ardhi na hatimaye wannachi walitoka na mapendekezo ya kukubali eneo hilo kuwa WMA.


Wanawake wapigwa marufuku kushinikizwa kuandamana.

Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Loliondo wakiandamana kupinga kamati wa utatuzi wa mgogoro wa pori tengefu.


BAADHI ya Wanawake  pamoja na watoto  wanatumiwa kama chambo  kwaajili ya  kusimamisha msafara wa Kamati ya Kukamilisha mchakato wa Utatuzi wa  Mgogoro wa Matumizi ya Ardhi kwenye Pori Tengefu la Loliondo.

Kutumika kwa wanawake hao ambao baadhi yao walikuwa na watoto wadogo migongoni kumebainika jana wakati kamati hiyo ilipokuwa ikiendelea kuangalia maeneo mbalimbali ya Pori hilo Tengefu la Loliondo lenye ukubwa wa kilomita 15,000 za mraba zilizoleta mgogoro kwa zaidi ya miaka 25 sasa.

Wanawake hao katika Kata ya Malambo na Kata ya  Arash,ambao kwa pamoja walibeba mabango  ya kuisihi Kamati hiyo kutenda haki mengine
yakimtuhumu Waziri wa Maliaisili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe
wakidai kuwapenda wanyamapori kuliko binadamu.


Baadhi ya wanwake hao ambao ni  Rehema Pascal na Lemnyaki John
walisimamisha mafara huo kwakuonyesha mabango yao yanayodai kutokubali kuhamishwa katika Pori hilo huku wengine wakipandisha mori na kupiga mayowe.


Baada ya Rc,Gambo kuyasoma mabango hayo aliwapa vipaza sauti ili
wayasome tena hapo ndipo waliposhindwa kuyasoma na kudai kuwa hawajui Kiswahili.
“Nani aliyewaandikia mabango haya wakati hamjui kusoma ,mnatumiwa na
viongozi wenu hukusu mgogoro huu ,msikubali kutumika maana hamjui
serikali inafanya hivi kwa nia ipi na wala serikali haina mpango wa
kuchukua ardhi hii bali tunachokifanya ni kujua hayo mnayoyasema yapo
kiuhalisia au la ili tukamilishe kazi yetu”.
Naye Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Felex Wandwe alisisitiza
aliwatoa hofu wananchi wa Kata saba za wilaya hiyo kutokubali kutumika
vibaya kwaajili ya Pori hilo kwani serikali inachofanya hivi sasa ni
kuchukua mapendekezo ya kamati hiyo kisha kuyawasilisha kwa Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa .


“Msikubali kutumiwa kwa maslahi ya wengine sisi tupo pamoja na
wawakilishi wenu na kabla ya kuanza zoezi hili walijua tunakuja
kufanya nini hivyo mtulie”.
Pia Katibu wa Kamati hiyo, Bahati Chisanza alisema kuwa ni vyema
wananchi wakajua kuwa serikali haichukui ardhi bali inachokifanya ni
kutaka kupanga matumzii bora ya ardhi ili kila mtu anufaike nayo.


Awali Mwenyekiti wa Kijiji cha  Malambo, Lazaro Mashele alitoa rai kwa
kamati hiyo kutoiingiza Kata hiyo ya Malambo katika matumizi bora ya
ardhi kwani kata hiyo haina mgogoro na Pori hilo bali ni wahifadhi
wazuri wa wanyamapori ingawa kata hiyo ni sehemu ya mazalia ya
wanyama.


“Tunawaomba wakuu kata hii isiingizwe katika  mgogoro huu kwani hatupo
ndani ya vijiji saba lakini pia kata hii inatumika kwaajili ya mazalia
ya wanyamapori ambao hatuna ugomvi nao”.


Aidha  Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gambo alisisitiza kuwa wamechukua maoni ya mwenyekiti huyo na watafanyia kazi maoni yote yaliyotolewa na
wananchi hao ,wahifadhi na wataalam wa ardhi kisha kuyawasilisha kwa
Waziri Mkuu Machi 25 mwaka huu.


Wakati huo huo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo
alitoa rai kwa wananchi hao  kutokubali kutumika kwa msalahi ya
wengine na kutoa rai kwa viongozi wa vijiji,madiwani na mashirika
yasiyo ya kiserikali kuacha mara moja kuwatumia wananchi kwaajili ya
kuwapotosha kuhusu Pori Tengefu la Loliondo.


Pia alisema polisi wataanza msako kwa wale wote ambao si raia wa
Tanzania wanaoishi Wilayani Loliondo huku akisisitiza kuwa wamemkamata
mtu mmoja ambaye ni mwanaume (hakumtaja jina) kwa kufanya vurugu
wakati kamati hiyo ilipokuwa ikifanya kazi yake katika kata mbalimbali
na muda wowote atafikishwa mahakamani wilayani humo.



Wednesday, January 25, 2017

ZIARA YA MKURUGENZI MTENDAJI WA SHIRIKA LA UNEP MKOANI ARUSHA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira bwana Erik Solheim alipowasili mkoani Arusha kwa ziara ya siku moja.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira Erik Solheim na viongozi wengine walipofanya kikao katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa kwenye picha ya pamoja na ugeni kutoka UNEP uliotembelea katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira bwana Erik Solheim akionyeshwa moja ya mahakama itakayotumika katika kusikiliza kesi mbalimbali na Mkuu wa mahakama ya Afrika kwa Arusha bwana Samuel Akorimo katika mahakama ya Afrika iliyopo Arusha

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira Erik Solheim akiangalia moja ya chanzo cha maji cha Olgilai wilayani Arumeru.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira Erik Solheim akizungumza na wadau wa utalii wa Mkoani Arusha juu ya masuala ya utalii na biashara haramu ya wanyapori.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira Bwana Erik Solheim akiangalia baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa na kiwanda cha Banana Investment alipotembelea kiwanda hicho kwa lengo lakuangalia mfumo wa usafishaji maji na utunzaji wa mazingira wa kiwanda hicho.

Friday, January 20, 2017

GAMBO AFANYA KIKOA NA WAFANYABIASHARA WADOGO WA MADINI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akiwa kwenye kikaona wafanyabiashara wadogo wa madini wa Jijini Arusha,kulia kwake ni Kamishina wa madini kanda ya Kaskazini Adam Juma na kushoto kwake ni kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha Charles Mkumbo.


Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo amewapiga marufuku polisi wa Mkoani Arusha kuwasumbua ovyo wafanyabiashara wadogo wa madini(Brokers) katika maeneo yao yakufanyia biashara bila kufuata utaratibu maalumu.
Ameyasema hayo alipokuwa akifunga kikao chake na wafanyabiashara hao katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kikiwa na lengo lakusikiliza kero zao na kuongeza ushirikiano baina ya wafanyabiashara hao na serikali yao ya Mkoa wa Arusha.
“Ninamwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kuanzia sasa kusimamisha zoezi hili lakuwasumbua hawa wafanyabiashara wadogo wa madini katika maeneo yao ya biashara bila kufuata taratibu”.
Aidha Gambo amewaagiza Kamishina wa Mamlaka ya mapato (TRA) Arusha na ofisi ya madini kanda ya Kansazini kuandaa mpango maalumu wakutoa elimu kwa wafanyabiashara wadogo wa madini wa Mkoa wa Arusha juu ya  utoaji wa leseni za madini na ulipaji wa kodi.
Alisema hayo baada ya wafanyabiashara hao kutoa malalamiko yakutoelewa taratibu za upatikanaji  wa leseni za madini na pia hawana elimu tosha juu ya ulipaji kodi kwani wengi wanaona wanatozwa kodi kubwa ambazo haziendani na hali halisi ya biashara zao wanazofanya.
Akisisitiza zaidi Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha,Charles Mkumbo amesema jeshi la polisi la Mkoa wa Arusha litaendelea kudumisha ulinzi na usalama kwa wananchi wote na mali zao.
Hivyo kawataka wafanyabaishara wadogo wa madini wa Mkoa wa Arusha kuwa na imani na jeshi lao la polisi kwani litaendelea kuwalinda wao na malizao na hata kwa wale waliokamatwa nakunyang’anywa madini yao, ofisi yake itafuatilia iliwanaostaili kurudishiwa watapewa mali zao.
Kamishina wa mamlaka ya mapato Arusha(TRA) bwana,Ambili Mbaluku amesema ni vizuri wafanyabaishara hao wakajitaidi kulipa kodi kadri ya mapato yao kwasabau serikali inategemea kodi hizo katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya jamii na wao watajitaidi kutoa elimu zaidi juu ya ulipaji kodi mzuri.
Pia kamishina wa madini kanda ya Kansazini Adam Juma amesema nivizuri wafanyabaishara hao wakakata leseni kwaajili yakuendesha shughuli zao kihalali huku wakitambulika na mamlaka husika kuwa niwafanyabiashara halali wa madini.
Mkuu wa Mkoa Gambo alimalizia kwakuwaadi kuendelea kukutana nao mara kwa mara angalau kila baada ya miezi mitatu na wafanyabiashara hao ilikufanya tathimini ya mambo mbalimbali ambayo wamekubaliana kama yatakuwa yamefanyiwa kazi na pia kama kutakuwa na mengine yaliyojitokeza.
Pia amewata wafanyabiashara hao wadogo wa madini kukaa pamoja na kamishina wa madini  wa kanda ili kuchagua uongozi wa mda wa chama chao kwakuwa uongozi uliopo ulionekana kutokubalika na wanachama  walio wengi, na uongozi huo utakuwa ukishughulikia matatizo na kero za wanachama wake kwa ukaribu zaidi.

Mmoja wa wafanyabiashara wadogo wa madini wa Jijini Arusha,Charles Liwa akizungumzia changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika biashara yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha na Viongozi wengine wa Mkoa wa Arusha (hawapo pichani).

Wafanyabiashara wadogo wa madini wa Jijini Arusha wakiwa kwenye kikao kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa ,Arusha.