RC Akiapishwa

Dk. John Pombe Magufuli akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha ,Mhe. Mrisho Gambo.

Ziara ya Waziri Mkuu wa Tanzania

Mhe. Mrisho Gambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa Ofisini kwake, Jijini Arusha.

JPM ,Mrisho Gambo Picha ya Pamoja

Dk. John Pombe Magufuli akipiga picha ya pamoja na mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.

Samia Suluhu Hassan akiwasili Jijini Arusha

Mkuu wa Mkoa Arusha, Mhe Mrisho Gambo Akimpokea Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Picha ya Pamoja

Mhe. Mrisho Gambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa.

Showing posts with label Afya. Show all posts
Showing posts with label Afya. Show all posts

Monday, November 19, 2018

IDARA YA DHARURA YAZINDULIWA MT.MERU

Mazingira wezeshi kwa watumishi wa umma ndio yatakuwa kichocheo cha wao kufanya kazi kwa bidii na  kwa weredi wa hali ya juu, hali hii itasaidia pia kuboresha huduma zitolewazo.

Haya yamesemwa na katibu mkuu wizara ya afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto  Dkt. Mpoki Ulisubisya alipokuwa akizindua idara ya huduma ya dharura na ajali katika hospitali ya mkoa ya Mt.Meru.

Dkt. Mpoki amesema, hatua zinazofanywa katika hospitali hiyo ni kubwa na nzuri sana hasa katika kuhakikisha huduma zinaboreshwa hasa kwa kuongeza majengo na huduma mbalimbali kama hiyo ya dharura.

Amesema serikali ipo tayari kuunga mkono juhudi hizo hasa kwa kuhakikisha wahuduma wa afya wanaongezwa na vitendea kazi pia
Akitoa taarifa fupi ya idara ya dharura mganga mfawidhi wa hospital Dokta Shafii Msechu amesema,ukarabati wa jengo la huduma za dharura limekaratabiwa kwa kushirikiana na taasisi ya Abbott Fund Tanzania.

Amesema lengo kubwa la kuanzisha idara hiyo ni kumaliza kabisa vifo vitokanavyo na magonjwa ya dharura na ajali.

Hata hivyo Dokta Msechu amesema mpaka sasa hospitali imeshakamilisha uchoraji wa michoro ya majengo ya waganjwa  wa nje,jengo la dharura, jengo la wagonjwa mahututi na vyumba vya upasuaji.

Zaidi ya shilingi bilioni 9 zitatumika katika ujenzi wa jengo la dharura na shilingi bilioni 22 zitatumika katika ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje na jengo la dharura.
 Akitoa shukrani  za dhati makamu mwenyekiti wa bodi ya hospitali ya Mt.Meru Hans Tosk, amesema bado hospitali inamahitaji mengi sana hivyo serikali na wadau wasichoke kuisadia hospitali pale mahitaji hayo yanapoombwa.

Pia, amesema bodi inafurahishwa sana na ushirikiano unaopatikana kutoka kwa serikali na kamshukuru sana Katibu Mkuu kwa kuwapa moyo wakuendelea  kuboresha huduma za hospitali.

Huduma ya idara ya dharura kwa mara ya kwanza nchini ilizinduliwa rasmi katika hospitali ya Muhimbili 2010 na mafanikio makubwa yalionekana baada ya kupunguza idadi kubwa ya vifo,hivyo kupelekea idara hii kuanzishwa katika hospitali vyingine.




Wednesday, November 14, 2018

KILA HALMASHAURI ITENGE SHILINGI 1000 KWA KILA MTOTO WA CHINI YA MIAKA 5

 Mkuu wa Mkoa wa Arusha ameziagiza halmashauri zote za mkoa huu kutenga kiasi cha shilingi 1000 kwa kila mtoto katika halmashauri kutoka katika mapato ya ndani ilikusaidia katika mfuko wa Lishe wa halmashauri.

Yamesemwa hayo na katibu tawala wa Mkoa Richard Kwitega kwa niaba ya mkuu wa mkoa alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja ya namna ya upangaji wa bajeti ya lishe katika mkakati wa lishe Kitaifa, amesema hali ya udumavu katika mkoa si nzuri sana upo kwa asilimia 36.

Amesema wahanga wakubwa ni watoto na wanawake ambapo watoto wengi wanaudumavu wa akili na mwili na wanawake wajawazito hujifungua watoto njiti au hupoteza maisha kabisa.

Hali za watoto kwa mkoa wa Arusha  kwa mwaka 2015/2016 watoto  wenye uzito mdogo kwa urefu ni  asilimia 6.5 na wenye uzito mdogo kwa umri ni asilimia 20.1 na watoto 57 kati ya 100 wana upungufu wa damu.
Amesema hali hii pia kwa akinamama wajawazito sio nzuri kwani wanawake wenye umri kati ya miaka 15 hadi 17, 14 kati ya 100 wana upungufu wa damu kwa takwimu za mwaka 2015/2016.

Akisisitiza zaida mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro amesema ifike wakati sasa elimu itolewe kwa kina juu ya ulaji mzuri wa vyakula mbadala vitakavyo ongeza virutubisho mbalimbali katika mwili badala ya kutumia madawa kwa wingi.

Amesema vyakula kama mbogamboga, matunda na vyakula vya nafaka vinavyoongeza madini, vitamin na virutubisho vingine mbalimbali yanayoitajika mwilini.

Pia, mpango mkakati wa lishe unaitaji bajeti ambayo utasimamia utekelezaji wake kwa kiasi kikubwa, amesema mafunzo hayo waliyopatiwa yatawasaidia kuwa na uwelewa mpana wa namna ya kusimamia shughuli nzima za lishe katika wilaya zao kwa ufasa.

Mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo wa kutengeneza bajeti za lishe katika mkoa wa Arusha  yaliyosimamiwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) yalifanyika kwa kuhusisha wilaya mbili ya Jiji la Arusha na Arusha Vijiji na kuendelea katika wilaya nyingine za Meru, Longido,Monduli,Karatu na Ngorongoro.


Friday, October 5, 2018

UGONJWA WA VIKOPE TISHIO

Viongozi wa Wilaya wa Mkoa wa Arusha wametakiwa kusimamia kikamilifu zoezi la utoaji dawa za ugonjwa wa vikope (Trakoma) kwenye maeneo yao kwa lengo la kuhakikisha ugonjwa huu unatokomezwa kabisa.

Akitoa rai hiyo alipokuwa akifungua semina ya mpango wa kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaombele  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, katibu tawala wa mkoa Richard Kwitega amesema ni vizuri viongozi wakajikita kwa nguvu zote katika zoezi hili lakutokomeza ugonjwa wa vikope kwenye maeneo yao.

“Ni rai yangu kwenu viongozi wote wa Wilaya na halmashauri kuhakikisha mnasimamia vyema zoezi hili lakutokomeza ugonjwa huu wa vikope katika maeneo yenu”.
Lengo la serikali nikutumia rasilimali chache kuthibiti magonjwa haya ambayo yanaonekana hayapewi kipaombele katika jamii yetu hivyo kila halmshauri ihakikishe inatenga fedha zakutosha zakusaidia upasuaji wa vikope.
Wilaya ya Karatu na halmashauri ya Arusha zimejitaidi kuhakikisha zimetokomeza ugonjwa wa vikope lakini bado katika halmashauri ya wilaya ya Longido na Ngorongoro, nguvu zaidi zinaitajika katika maeneo haya.

Kwa mkoa wa Arusha watu takribani 1076 wameshafanyiwa upasuaji wa vikope katika halmshauri zote za wilaya na magonjwa yanayoongoza katika mkoa huu ni ugonjwa wa Kichocho ,Minyoo ya Tumbo na vikope.

Amewataka washiriki wa semina hiyo kuhakikisha kuwa elimu wanayoipata katika mafunzo hayo wakaitumie vizuri katika kutokomeza magonjwa hayo kwenye maeneo yao.
Nae mratibu wa magonjwa yalisiyopewa kipaombele  kutoka Wizara ya Afya, maendeleo ya jamii,jinsia, wazee na watoto Dokta Upendo Mwingira, amesema takribani magonjwa 17 yasiyopewa kipaombele yapo katika bara la Asia, Amerika ya Kusini na Kusini mwa jangwa la Sahara.

Amesema magonjwa mengine ambayo hayapewi kipaombele ni AIDS, TB, Malaria, Kuumwa na nyoka,Matende, Mabusha, Usubi na Ukoma.
Amezitaja athari mbalimbali zinazotokana na magonjwa haya ni kama mgonjwa kupata ulemavu wa mda mrefu, Udumavu kwa watoto,kupunguza uwezo wa kufanya kazi,unyanyapaaji, kansa ya kibofu cha mkojo, upofu na presha ya ini.


Akitoa taarifa fupi ya ugonjwa wa vikope kwa mkoa wa Arusha Dokta Mwanahawa Kombo kutoka hospitali ya Mkoa Mt. Meru, amesema jumla ya wagonjwa 1076 wameshapasuliwa vikope na halmashauri ya Monduli imefanya vizuri katika kukabiliana na ugonjwa huu kati ya halmashauri 2 za Longido na Ngorongoro.
Semina hii hufanyika kila mwaka kwa lengo la kutoa elimu na takwimu sahihi za hali  halisi ya magonjwa yasiyopewa kipaombele nchini.

Semina hii hufanyika kila mwaka kwa lengo la kutoa elimu na takwimu sahihi za hali  halisi ya magonjwa yasiyopewa kipaombele nchini

Tuesday, September 25, 2018

TATIZO LA KUPOTEZA KUMBUKUMBU NI UGONJWA NA SIO KAWAIDA KWA WAZEE




Mkoa wa Arusha kwa mara ya kwanza umeweza kuadhimisha siku ya ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu kwa wazee wenye umri kuanzia miaka 60 zoezi hili limefanyika katika hospitali ya mkoa Mt.Meru.

Akitoa taarifa ya maadhimisho hayo yaliambatana na upimaji wa magonjwa mengine kama Kisukari, Presha na Uzito, mwanasaikolojia kutoka hospitali ya Mkoa Mt.Meru bwana Ssenku Shafic Mohamed, amesema zoezi hilo limechukua mda wa wiki nzima.

Na lengo kubwa lilikuwa nikuwapima wazee wenye umri kuanzia miaka 60 na kuendelea ili wajitambue hali yao ya kumbukumbu na magonjwa mengine yasiyoambukiza kama Kisukari,Presha na Uzito.

Aidha, kutokana na zoezi hilo bwana Ssenku amesema wameweza pia kugundua magonjwa mengine kama mtoto wa jicho na tezi dume kwa wazee wanaume.

“Katika hali ambayo hatukitarajia tumeweza kugundua pia ugonjwa wa mtoto wa jicho ambapo kati ya wagonjwa 10 waliokuja hapa watatu kati yao walikuwa wamegundulika na tatizo hilo na pia  ugonjwa wa tenzi dume ambapo kati ya wagonjwa 10 wawili wamegundulika na tatizo hilo”.


Amesema wamefanikiwa pia kutoa ushauri wa vyakula sahihi vinavyowafaa wazee na aina ya mazoezi ili kuhakikisha afya zao zinaimarika na wanajikinga na magonjwa mbalimbali hasa la kupoteza kumbukumbu ambalo lina sadikika ni kawaida kwa wazee lakini kitaalamu ni ugonjwa ambao ukipatiwa matibabu mapema hospitali unatibika.

Maadhimisho hayo yanafanyika kila mwaka Septembea 21 duniani na kwa mwaka huu Tanzania kupita mkoa wa Arusha imeadhimisha siku hii kwa mara ya kwanza kwa kushirikiana na nchi nyingine kama vile Mauritius, Nigeria, Zimbabwe, Madasca na Tunisia.

Friday, September 14, 2018

MILIONI 469 ZATUMIKA KATIKA UJENZI WA KITUO CHA FYA

Jengo la kituo cha afya kata ya Mto wa Mbu wilayani Monduli,kilichojengwa na serikali kwa kushirikiana na nguvu za wananchi.



Milioni 469 zimetumika katika ujenzi wa kituo cha afya Mto wa Mbu wilayani Monduli.

Akisoma taarifa ya mradi huo Mganga mkuu wa kituo cha afya Dr. Emma Agostino Msofe, amesema ujenzi wa kituo hicho ulianza mwaka 2017 baada ya serikali kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 400.

Pia fedha nyingine zimetoka halmashuri kiasi cha shilingi milioni 30 na wananchi  wamechangia milioni 39.

Ujenzi wa kituo hicho cha afya unaendelea na mpaka sasa majengo yaliyojengwa ni  jengo la upasuaji, jengo la wazazi,jingo kufulia,nyumba ya utumishi,vyoo vya nje na matenki ya kuhifadhia maji.

Amesema kituo hicho cha afya kitawasaidia wananchi kupata huduma bora za afya na katika mazingira bora.

Nae kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa ndugu. Charles Francis Kabeho, amesema wananchi wanatakiwa kukitunza kutuo hicho kwa umakini na pia amewataka watumishi watoe huduma bora na kwa weridi kwa wananchi.


Mwengi wa Uhuru ulianza mbio zake mkoani Arusha Mnamo Septamba 12 katika wilaya ya Ngorongoro kisha wilaya ya Karatu na sasa unaendelea katika wilaya ya Monduli.

Kiongozi wa mbio za Kitaifa ndg. Charles Francis Kabeho, akizundua kituo cha afya cha Mto wa Mbu wilayani Monduli.


Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Charles Kabeho ( mwenye sare ya gwanda) akiwa na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Monduli wakitoka kizindua mradi wa kituo cha afya cha mto wa Mbu.


Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Charles Kabeho akikagua mradi wa kuchakata chakula cha mifugo klatika kijiji cha Mungere kata ya  Esilalei wilayani Monduli.


Wednesday, August 29, 2018

MWANAUME JALI AFYA YAKO, PIMA

Mkuu wa Wilaya  ya Monduli Idd Kimanta (katikati) akiwa na viongozi mbalimbali na wadau wa sekta ya afya katika uzinduzi wa kampeni ya "Furaha Yangu",Meserani wilayani Monduli.

Watakaogundulika wana maambukizi ya virusi vya UKIMWI wanatakiwa kuwaleta wenza wao wapimwe  pia ili waweze kujitambua na kuishi mda mrefu.

Ameyasema hayo Mkuu wa Wilaya ya Monduli  Idd Kimanta kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katika uzinduzi wa kampeni ya upimaji wa virusi vya UKIMWI kwa hiari ijulikanayo kama “FURA YANGU”.

Gambo amesema bado idadi ya wanaume wanaoenda kupima ni ndogo sana ukilinganisha na wanawake, hivyo nguvu za uhamasishaji inaitajika zaidi kwa wanaume.

Ikiwezekana hata kutumia mikusanyika kama sehemu za ibada na maeneo ya starehe ili kuweza kuwapata wanaume wengi na kuwahamasisha wajitokeze zaidi.

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Idd Kimanta akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya Furaha Yangu akiwa na (kulia) ni Mganga Mkuu wa Wilaya Dr. Titus Mmasi, wilayani Monduli.

Pia wataalamu wanatakiwa kuongeza zaidi wigo wa utoaji huduma hii kama kutoa ushauri nasaha na kuwahamasisha wagonjwa wapime kwa hiari.

Akitoa takwimu za hali ya maambukizi kwa mkoa wa Arusha Mganga mkuu wa mkoa Vivian Wonanji, amesema kwa mwaka 2011/2012 hali ya maambukizi imeshuka sana kutoka 3.2% hadi 1.9 kwa mwaka 2017/2018.

Amesema hali hii ni nzuri sana kwa mkoa wetu lakini hatutakiwi kupunguza nguvu hii ya upimaji wa hiari na matumizi ya dawa kwa wagonjwa kwani mpaka sasa waliogundulika na VVU ni 52.2% wenye umri kati ya miaka 15-64 ambapo wanaume ni 45.3%na wanawake ni 55.9%.

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Idd Kimanta akipata maelezo kutoka kwa mganga mkuu wa Wilaya ya Monduli Dr. Titus Mmasi wakati wa kutembelea mambanda mbalimbali ya upimaji wa kampeni ya Furaha Yangu,Wilayani Monduli.

Hali hii inaonesha kuwa bado jitihada inaitajika kuhamasisha wanaume wajitokeze zaidi katika upimaji na sio upimaji tu hata pia matumizi ya dawa kwani kati ya wagonjwa 90.9% wanaotumia dawa wanaume ni 86.2% tu na wanawake ni 92.9%.

Aidha, amesisitiza zaidi hata katika hatua ya kufubaisha VVU kwa wagonjwa wanaotumia dawa bado msukumo ni mdogo kwa wanaume kwa 84% kati ya wagonjwa 87.7%.

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Idd Kimanta akipima msukumo wa damu (Presha) kama ishara ya uzinduzi wa kampeni ya Furaha Yangu, Wilayani Monduli.

Kupitia kampeni hii ya Furaha yangu yenye ujumbe wa Pima,Jitambue,Ishi itasaidia zaidi kuwahamasisha wanaume kupima kwa hiari.

Akitoa takwimu za upimaji katika kampeni hii kuanzia Agosti 17, 2018 wilayani Monduli mwakilishi kutoka Mkapa Foundation David Mnkhally amesema,jumla ya watu 5,730 ndio wameweza kupima na 29 ndio wamegundulika na maambukizi ya VVU.

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Idd Kimanta akizungumza na wananchi wa Meserani (Hawapo Pichani) katika uzinduzi wa kampeni ya Furaha Yangu,Wilayani Monduli.

Ikiwa katika kata ya Monduli Juu jumla ya watu 2.987 wamepima na kati yao wanaume ni 1,206 sawa na 40.3% na wanawake ni 1,781 sawa na 59.6% na kata ya Meserani waliopima ni 2.743,wanaume ni 1,378 sawa na 50.2% na wanawake ni 1,365 sawa na 49.7%.

Kampeni hii ya Furaha Yangu ilizinduliwa rasmi mnamo Juni 2018 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jijini Dodoma, na kwa mkoa wa Arusha zimezinduliwa rasmi Agosti 28, 2018 katika kata ya Meserani wilayani Monduli na itaendelea katika wilaya ya Ngorongoro.

Mganga Mkuu wa Mkoa Dr. Vivian Wonanji akizungumza katika uzinduzi wa kampeni ya "Furaha Yangu" Wilayani Monduli.


Mwakilishi kutoka Taasisi ya Mkapa Foundation David Mnkhally akisoma taarifa fupi kwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni ya "Furaha Yangu",Wilayani Monduli.


Monday, July 23, 2018

UZINDUZI WA KAMPENI YA UPIMAJI BURE YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA.

Baadhi ya watumishi wa umma wakipata semina  ya magonjwa sugu yasiyoambukiza katika viwanja vya Azimio Arusha.



Mganga Mkuu wa Mkoa Dr. Vivian Wonanji akipimwa msukumo wa damu (Pressure) kama ishara ya uzinduzi wa kampeni ya upimaji magonjwa sugu yasiyoambukizwa kwa Mkoa wa Arusha.


Shekh Mkuu wa Mkoa wa Arusha  Shaban Bin Juma ,akipimwa msukumo wa damu katika kampeni ya upimaji bure wa magonjwa sugu yasiyoambukiza, Jijini Arusha.


Thursday, May 31, 2018

MPINA AFUNGUA MAONESHO YA WIKI YA MAZIWA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhanga Mpina (wa pili kulia) akikata utepe kuzindua wiki ya maziwa Kitaifa kwenye uwanja wa maonyesho ya Kilimo na  Mifugo Nanenane Njiro,kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na viongozi wa Baraza la Kilimo na Bodi ya Maziwa.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhanga Mpina akitoa hotuba yake kwenye uzinduzi wa wiki ya Maziwa Kitaifa kwenye uwanja wa maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro jijini Arusha.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi mheshimiwa Luhanga Mpina, ameiagiza bodi ya maziwa kwa kushirikiana na baraza la kilimo Tanzania kuandaa maonyesho ya kimataifa ya wiki ya maziwa badala kila mwaka kuadhimisha yakitaifa tu.
Ameyasema hayo alipokuwa akufungua maonyesho ya 21 ya wiki ya maziwa kitaifa, yaliyofanyika katika viwanja vya Themi Njiro jijini Arusha.
Amewataka kuendelea kusimamia sheria na kanuna za maziwa zinazotumika katika kila nchi, kwani soko la maziwa linapanuka kwa kasi sana.
Aidha, amesisitiza kuwa serikali inaendelea kuhakikisha inabadilisha sheria na kanuni ambazo zinaonekana hazina tija katika sekta hiyo, hii itasaidia sana katika uboreshaji wa soko la maziwa ndani na nje ya nchi.
Amewahasa wafugaji waendelee kutumia ufugaji wa kisasa kwani utaongeza uzalishaji wa maziwa kwa wingi nakutoa fursa zaidi za masoko kwa nchi za nje.
Nae Mkuu wa Mkoa wa Arusha ameipongeza sana bodi ya maziwa kwa kufanikisha madhimisho hayo ya wiki ya maziwa na amewataka wazalishaji wazingatie zaidi sheria na kanuni za ndani na nje ya nchi ili kuepuka usumbufu usiokuwa wa lazima.
Magreti Kihumbuli mwakilishi kutoka bodi ya maziwa Kenya, ameishukuru bodi ya maziwa Tanzania kwa kuwapa mwaliko wakushiriki maonyesho hayo.
Amesema anatagemea kujifunza mambo mengi katika maonyesho hayo na hata pia waonyeshaji wa Tanzania watajifunza mengi kutoka kwao na hii itasaidia kuongeza uhusiano bora kati ya nchi hizi.
Luge Kawaga ni mwakilishi kutoka mamlaka ya endelezaji wa maziwa nchini Uganda, amesema maonyesho hayo yatasaidia kubadilisha elimu baina ya nchi hizo tatu.
Maonyesho ya wiki ya maziwa kitaifa yanafanyika mkoani Arusha kwa siku 3 ambapo makapuni takribani 40 yakiwemo ya kigeni yameweza kushiriki maonyesho hayo.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhanga Mpina akiwapa wanafunzi wa Shule ya Msingi Baraa ya Jijini Arusha baada ya kuzinduawiki ya Maziwa Kitaifa kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro,kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.


Meneja wa Kampuni ya Milkcom maarufu Dar Fresh,Tunnu Mssika akimpa maelezo Waziri wa Mifugo na Uvuvi wakati akikagua mabanda ya waoneshaji bidhaa mbalimbali zinazotokana na Mifugo.








Wednesday, May 16, 2018

VITUO VYA AFYA KUJENGWA LONGIDO

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa na Mbunge wa jimbo la Longido Dkt. Steven Kiruswa, wakishirikiana na wananchi wa kata ya Ketumbeini kukusanya mawe kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha kata hiyo,wilayani Longido.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema wananchi wa kata ya Kimokouwa na Namanga kwa ujumla hawana haja yakupata matibabu tena kutoka nchi jirani ya Kenya.
Aliyasema hayo alipokagua ujenzi wa kituo cha afya cha Eworendeke katika kata ya Kimokouwa wilayani Longido.
Gambo amesema kwa mda mrefu sana wananchi wa Namanga kwa ujumla walikuwa wanapata hadha yakufuata huduma ya matibabu Longido mjini au nchi jirani ya Kenya na hivyo kufanya wagonjwa wengi kutembea umbali mrefu.
Amesema kituo hicho cha afya kimepata mgao wa shilingi milioni 700 kutoka serikalini na wananchi wanachangia nguvu kazi katika kukijenga na mpaka sasa kiasi cha milioni 400 ndio kimeshatumika na ujenzi unaendelea.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akikagua ujenzi wa kituo cha afya cha Engarenabor kitakacho gharimu kiasi cha milioni 200 mpaka kukamilika.

Gambo amesema mbali na serikali kutoa kiasi hicho cha fedha bado bajeti ya ununuzi wa madawa umeongezwa kutoka bilioni 31 hadi bilioni 269 kwa mwaka huu wa fedha, na hii itasaidia huduma ya madawa kupatikana kiurahisi katika kila kituo cha afya na hospitali zote nchini.
Kituo cha afya cha Eworendeke kinatarajia kukamilika Agosti 2018 na huduma zote zitapatikana zikiwemo huduma za  upasuaji na x-ray, hivyo itarahisisha matibabu kwa wananchi wote wa Namanga.
Mkuu wa Wilaya ya Longido Daniel Chongolo,amesema asilimia 27 ya wajawazito walikuwa wanajifungulia katika vituo vya afya kwa wilaya nzima na idadi imeongezeka kufikia asilimia 35.
Chongolo amesema ongezeko hili litasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto katika wilaya yake.

Ujenzi wa kituo cha afya cha Eworendeke Namanga unaondelea na kituo kitagharimu kiasi cha milioni 700 fedha kutoka serikalini,kituo kipo wilayani Longido.

Mgaga mkuu wa Mkoa Dokta Vivian Wonanji,amesema serikali imeshatenga kiasi cha fedha cha milioni 200 kwa ajili ya manunuzi ya vifaa kwa vituo vyote vya afya na hospitali kwa mkoa mzima na anaendelea na zoezi la kuongeza watumishi katika sekta ya afya.
Amesema agizo la serikali ni kuhakikisha vituo vyote vya afya vinakuwa na huduma ya x-ray, hivyo katika kituo hicho wanajenga chumba maalumu kitakachotoa huduma hiyo kwa wananchi wote wa Namanga.
Akitoa shukurani zake za dhati kwa serikali bwana Hassan Hamis ambae ni mkazi wa Namanga amesema kweli kituo hicho cha afya kitasadia kuondokana na hadha waliyokuwa wanaipata kufuata matibabu kwa umbali mrefu, na pia itapunguza vifo vilivyokuwa vinatokana na umbali huo.
Gambo anaendelea na ziara yake katika wilaya ya Longido ambapo ametembelea kituo kingine cha afya cha  Engarenaibor kilichogharimu kiasi cha milioni 200, pia ameshiriki ujenzi wa kituo cha afya cha kata ya Ketumbeine.

Friday, April 27, 2018

KATIBU TAWALA AKUTANA NA WAJUMBE KUTOKA BENKI YA DUNIA

Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega, akiwa na wajumbe kutoka Benki ya Dunia ofisini kwake pamoja na wataalamu kutoka katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Arusha.


Kiongozi wa ujumbe kutoka Benki ya Dunia Bwana Nicholas Soikan (mwenye suti ya blue) akiandika maelezo yaliyokuwa yanatolewa na wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa (Hawapo pichani),katika ofisi ya katibu tawala,Arusha.


Katibu Tawala Bwana Richard Kwitega,akiongoza kikao kilichowakutanisha ujumbe kutoka Benki ya Dunia na wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Arusha.



Taarifa ya Mkuu wa Mkoa Arusha katika kipindi cha TUNATEKELEZA.

UZINDUZI WA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI



Ushirikishwaji katika kutoa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kutoka katika sekta mbalimbali hasa za dini,kisiasa na kabila ni muhimu sana.

Akiyasema hayo kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro amesema kuwa zoezi hili lisichanganywe na mambo ya siasa bali sekta hizo zitumike kutoa elimu zaidi.

Ameyasema hayo alipokuwa akizindua utoaji wa chanjo hiyo kimkoa katika shule ya msingi Ngarenaro,ambapo amesema wasichana 21,198 watapatiwa chanjo hiyo kwa mkoa wa Arusha.





Aidha,saratani ya mlango wa kizazi niya pili baada ya saratani ya matati, kwa asilimia 38 na niya kwanza kwakuwa na vifo vingi kwa Tanzania, ikifuatiwa na saratani ya shingo ya kizazi kwa asilimia 32.8,saratani ya koo asilimia 10.9 na saratani ya tezi dume kwa asilimia 2.1.

Chanjo hii inapatikana katika vituo vyote vya afya na ni bure kwa wasichana wenye umri wa miaka 14.Kila mwaka wanawake 466,000 wanathibitika kuwa na saratani ya mlango wa kizazi.




Akizungumza kwa niaba ya katibu tawala wa mkoa wa Arusha,mganga mkuu wa mkoa wa Arusha Vivia Tomothy Wonanji, amesema kila mtoto aliyefikisha miaka 14 anatakiwa kupatiwa chanjo hii na itarudiwa baada ya miezi sita ya chanjo ya kwanza.

Amewashukuru wadau wote walioshirikiana na Serikali katika kufanikisha upatikanaji wa chanjo hii na bure nchi nzima.



Amewatoa shaka wananchi wote kuwa chanjo hiyo ni salama kabisa na elimu itaendelea kutolewa kwa watu ili kuwaondoa wasiwasi wakuwa chanjo hii inaharibu kizazi.

Chanjo hii yakuzuia saratani ya mlango wa kizazi ilizunduliwa hivi karibuni nchini na waziri wa afya,maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Ummi Mwalimu na kufuatia uzinduzi mdogo katika mikoa na halmashauri zote ambapo kwa Arusha ilizinduliwa mnamo Aprili 25,2018.