RC Akiapishwa

Dk. John Pombe Magufuli akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha ,Mhe. Mrisho Gambo.

Ziara ya Waziri Mkuu wa Tanzania

Mhe. Mrisho Gambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa Ofisini kwake, Jijini Arusha.

JPM ,Mrisho Gambo Picha ya Pamoja

Dk. John Pombe Magufuli akipiga picha ya pamoja na mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.

Samia Suluhu Hassan akiwasili Jijini Arusha

Mkuu wa Mkoa Arusha, Mhe Mrisho Gambo Akimpokea Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Picha ya Pamoja

Mhe. Mrisho Gambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa.

Showing posts with label Uchumi. Show all posts
Showing posts with label Uchumi. Show all posts

Tuesday, December 4, 2018

LIPENI KODI KWA MAENDELEO YA TAIFA-MAGUFULI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli, ameitaka mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kufanya uchunguzi wa kina wa sababu inayosababisha wafanyabiashara kutokulipa kodi.

Aliyasema hayo alipokuwa akihutubia wananchi wa kata ya Kimnyaki wilayani Arumeru mkoani Arusha baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa maji safi na usafi wa mazingira wa Jiji la Arusha na baadhi ya maeneo ya wilaya ya Arumeru.

Magufuli amesema kuna baadhi ya wafanyabiashara wanawatumia wafanyabiashara wadogo (wamachinga) kuwauzia bidhaa zao ingali wao wanafunga maduka yao kwa lengo la kukwepa kulipa kodi.

Nchi inaendeshwa kwa kodi za wananchi hata mradi huu wa maji niwa mkopo wa riba ya bei nafuu kutoka benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na wananchi ndio mtalipa deni hili kwa kulipa kodi.

Amewahasa wananchi kulipa kodi kwa ustawi wa maendeleo ya nchi kwani miradi mingi ya maendeleo inategemea kodi za wananchi,hivyo niwatake wamachinga kutokukubali kutumiwa na wafanyabiashara wakubwa ili wakwepe kodi.

Pia,ameiagiza TRA kuangalia tena viwango vyake vya tozo za kodi kwani huwenda viwango ni vikubwa sana vinavyowafanya wafanyabiashara wengi kukwepa kulipa kodi kwani ni bora kuwa na viwango vidogo ili wengi walipe kuliko viwango vikubwa vinavyowashinda kulipa.

Amesema elimu pia inaitajika kwa wananchi juu ya umuhimu wa ulipaji kodi kwa wananchi na maendeleo ya nchi kwa ujumla.
Magufuli aliweka jiwe la msingi katika mradi wa maji utakaogharimu kiasi cha bilioni 520 mpaka kukamilika na utakuwana na uwezo wakuzalisha lita million 208 kwa siku.



Amewahasa wananchi kulipa kodi kwa ustawi wa maendeleo ya nchi kwani miradi mingi ya maendeleo inategemea kodi za wananchi,hivyo niwatake wamachinga kutokukubali kutumiwa na wafanyabiashara wakubwa ili wakwepe kodi.

Pia,ameiagiza TRA kuangalia tena viwango vyake vya tozo za kodi kwani huwenda viwango ni vikubwa sana vinavyowafanya wafanyabiashara wengi kukwepa kulipa kodi kwani ni bora kuwa na viwango vidogo ili wengi walipe kuliko viwango vikubwa vinavyowashinda kulipa.

Amesema elimu pia inaitajika kwa wananchi juu ya umuhimu wa ulipaji kodi kwa wananchi na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Magufuli aliweka jiwe la msingi katika mradi wa maji utakaogharimu kiasi cha bilioni 520 mpaka kukamilika na utakuwana na uwezo wakuzalisha lita million 208 kwa siku.

Sunday, December 2, 2018

RAIS MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli leo ameweka jiwe la msingi katika mradi wa maji safi na usafi wa mazingira wa jijini Arusha katika kata ya Kimnyaki wilayani Arumeru.

Amesema wananchi wote ambao wanaishi katika vyanzo vya maji na ambao mradi utawapitia katika maeneo yao watapatiwa maji kwanza wao kabla yakusambazwa maeneo mengine.

Magufuli amesema mradi huu ambao utawanufaisha wananchi wa jiji la Arusha kwa kiasi kikubwa lakini hata pia wananchi wa kata ya Oldonyosambu wilayani Longido pia nao wapatiwe maji kutoka kwenye mradi huo.


“Jana nimesimamishwa  njiani na wananchi wa Oldonyosambu na kero yao kubwa ilikuwa ni ukosefu wa maji safi kwani wanayoyatumia sasa yama madini ya Floride kwa wingi hivyo yanawaadhiri sana wao na watoto wao.”
 Amesema fedha zilitumika katika ujenzi wa mradi huo wa maji ni mkopo wa riba nafuu kutoka Benk ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), hivyo wananchi wote wanajukumu la kulilipa deni hilo.

Magufuli amewataka wakandarasi wa mradi huo ambao wapo 10 wafanye kazi kwa bidii usiku na mchana ili kuhakikisha mradi unakamilika ifikapo mwanzoni mwa Juni 2020 na wananchi waweze kupata maji kwa haraka.
Waziri wa maji na umwagiliaji Pro Makame Mbalawa amesema, hitaji la maji kwa mkao wa Arusha ni lita milioni 94 kwa siku lakini mradi huo unauwezo wakuzalisha lita milioni 208 kwa siku hivyo  ni zaidi ya mara 4 ya uhitaji wa Mkoa.
Akisoma taarifa ya mradi huo Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya maji safi na taka Arusha Enginia Ruth Koya amesema, mradi huo hadi kukamilika utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 520.
Amesema mradi huo utakuwa na uwezo wa kuzalisha lita milioni 208 kwa siku tofauti na hali ya sasa ambayo ni lita milioni 40 kwa siku huzalishwa sawa na asilimia 42 na hitaji la mkoa ni lita milioni 94 kwa siku.

Koya amesema kutokana na ongezeko hilo la uhitaji wa maji wa takribani asilimia 100 hadi ifikapo 2020 mkoa wa Arusha utakuwa na uwezo wakuwahudumia watu takribani milioni 1.

Mbali na mafanikio hayo amesema changamoto kubwa wanayokutana nayo ni ugumu wa kupata njia zakulaza mabomba hasa katika maeneo ambayo hayajapimwa,pia gharama kubwa za fidia wanazopaswa kuwalipa wananchi.

Rais Magufuli amefanya ziara yake katika mkoa wa Arusha kwa siku 2 kuanzia Desemba 1 hadi Desemba 2,2018 nakuweza kufungua kituo cha malipo ya forodha cha pamoja Namanga wilayani Longido na kumalizia na uwekaji jiwe la msingi katika mradi mkubwa wa maji safi na mazingira wa jijini Arusha.


MAGUFULI NA KENYATA WAFUNGUA KITUO CHA FORODHA CHA PAMOJA


Kituo cha forodha cha mpaka wa Namanga mkoani Arusha kinatarajia kukusanya mapato ya kiasi cha bilioni 53 kwa mwaka 2019.

Yamesemwa hayo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akifungua kituo cha pamoja cha forodha kati ya Tanzania na Kenya katika mpaka wa Namanga Arusha.

“Vituo hivi vya huduma ya pamoja vinasaidia kurahisisha usafiri, kukuza biashara na utalii na urahisi kwa wananchi wetu kuvuka mpakani mara  kwa mara.”

Amesema nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinachangamoto ya kuwa na vikwanzo vya kibiashara vinavyopeleka uchumi wa nchi hizi kudolola ukilinganisha na mabara mengine kama ya Amerika.

Kutokana na changamto hiyo nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zikachukua uwamuzi wa kuanzisha vituo vya forodha vitakavyo saidia kukuza biashara kwa nchi husika.

Nae Rais wa Jamhuri ya Kenya Uhuru Kenyata amesema, kituo hicho kiwe chachu ya kuwasaidia wafanyabiashara wadogo kukuza biashara zao kwani wao ndio msingi wa uchumi katika nchi zetu.
Kenyata amesema ni wajibu wa watumishi wa kituo hicho kuwasaidia na kuwajali wafanyabiashara hao wadogo na wao wafanyabiashara wafuate sheria za nchi husika na biashara zao ziwe halali.

Amesema jukumu la serikali ni kuhakikisha wananchi wake wanafanya biashara kwa haki na uhuru bila ubuguzi wowote.

Gavana wa jimbo la Kajado Joseph Oleleku, alisema ili nchi hizi mbili ziweze kunufaika na fursa za biashara amekuwa akifanya mikutano ya mara kwa mara ili kuhakikisha wafanyabaishara wanapata haki zao na wanafanya biashara zao kwa uhuru.

Akitoa neno la ukaribisho mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema,Mkoa umeendelea kuhakikisha usalama wa mpaka huo unaimarika kwa kiasi kikubwa kwa kuongeza ulinzi wa kutumia mbwa.

Gambo amesema mbali na huduma nzuri iliyopo katika mpaka huo kuna changamoto ya ukosefu wa scanna kwa ajili ya ukaguzi wa magari makubwa, ukosefu wa huduma ya upimaji wa ubora wa bidhaa  zinazoingia na kutoka mpakani.

Magufuli yupo katika ziara ya siku 2 mkoani Arusha ambapo amefungua kituo cha pamoja cha forodha na ataweka jiwe la msingi katika mradi mkubwa wa maji katika jiji la Arusha na wilaya ya Arumeru.

Friday, November 23, 2018

TUNZENI VYANZO VYA MAJI

 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, imeiagiza bodi ya Mamlaka ya maji safi na Usafishaji Mazingira ya jiji la Arusha AUWSA kuweka kipaombele katika utunzaji wa vyanzo vya maji viliyopo katika mlima Meru.

Ameyasema hayo alipokuwa  katika ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya maji katika jiji la Arusha.

“Nimewahi kusikia wataalam wa maji wakisema Vita ya Tatu ya dunia itahusisha kugombea maji,ninaomba sisi tuanze kujihami kwa kutunza vyanzo vyetu vya maji.Niitake bodi ya AUWSA kuandika andiko la mradi ambalo tutalipigia debe katika ofisi ya Makamu wa Rais inayoshughulikia Mazingira ili kuweza kupata ufadhili wa kampeni yetu hii ya utunzaji wa vyanzo vya maji”.

Gambo alisema,itakuwa haina maana kutumia kiasi kikubwa cha fedha za serikali katika uboreshaji wa huduma za maji na baada ya miaka michache ijayo vyanzo vyote vikauke.
 Nae Mkurugenzi wa Mmlaka ya Maji safi na usafirishaji (AUWSA) Mhandisi Ruth Koya amesema, mradi huo utakamilika June 2020 na Arusha itanufaika sana na mradi huo kwakuwa  ukosefu wa maji utakuwa historia.

Amesema tayari wakandarasi wameshaanza kusambaza mtandao wa maji safi na taka kwa kuweka mabomba ya kisasa yanayoendana na mahitaji ya sasa.

Aidha, amesema mpaka mradi huu ukamilike upatikanaji wa maji katika jiji la Arusha utafikia asilimia 100 tofauti na hali ya sasa ambapo ni asilimia 44 tu ya wananchi ndio wanapata maji safi.
 Ruth alisema, uzalishaji wa maji utaongezeka kutoka wastani wa lita milioni 40 hadi lita milioni 200 kwa siku na upotevu wa maji utashuka toka asilimia 40 za sasa hadi wastani wa asilimia  25.

Mwenyekiti wa bodi ya AUWSA, Dk. Richard Masika ameipongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuweza kutoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 520 kupitia mkopo wa riba nafuu kutoka benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika kufanikisha mradi huu mkubwa na ametoa rai kwa wananchi wa Arusha kuitunza muindombinu iliyopita katika maeneo yao kwa ajili ya manufaa ya leo na baadae.

Gambo yupo katika ziara ya siku 3 katika wilaya ya Arusha, Arumeru na Longido akikagua miradi ya maji inayoendeleo katika maeneo hayo.


Wednesday, November 14, 2018

KILA HALMASHAURI ITENGE SHILINGI 1000 KWA KILA MTOTO WA CHINI YA MIAKA 5

 Mkuu wa Mkoa wa Arusha ameziagiza halmashauri zote za mkoa huu kutenga kiasi cha shilingi 1000 kwa kila mtoto katika halmashauri kutoka katika mapato ya ndani ilikusaidia katika mfuko wa Lishe wa halmashauri.

Yamesemwa hayo na katibu tawala wa Mkoa Richard Kwitega kwa niaba ya mkuu wa mkoa alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja ya namna ya upangaji wa bajeti ya lishe katika mkakati wa lishe Kitaifa, amesema hali ya udumavu katika mkoa si nzuri sana upo kwa asilimia 36.

Amesema wahanga wakubwa ni watoto na wanawake ambapo watoto wengi wanaudumavu wa akili na mwili na wanawake wajawazito hujifungua watoto njiti au hupoteza maisha kabisa.

Hali za watoto kwa mkoa wa Arusha  kwa mwaka 2015/2016 watoto  wenye uzito mdogo kwa urefu ni  asilimia 6.5 na wenye uzito mdogo kwa umri ni asilimia 20.1 na watoto 57 kati ya 100 wana upungufu wa damu.
Amesema hali hii pia kwa akinamama wajawazito sio nzuri kwani wanawake wenye umri kati ya miaka 15 hadi 17, 14 kati ya 100 wana upungufu wa damu kwa takwimu za mwaka 2015/2016.

Akisisitiza zaida mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro amesema ifike wakati sasa elimu itolewe kwa kina juu ya ulaji mzuri wa vyakula mbadala vitakavyo ongeza virutubisho mbalimbali katika mwili badala ya kutumia madawa kwa wingi.

Amesema vyakula kama mbogamboga, matunda na vyakula vya nafaka vinavyoongeza madini, vitamin na virutubisho vingine mbalimbali yanayoitajika mwilini.

Pia, mpango mkakati wa lishe unaitaji bajeti ambayo utasimamia utekelezaji wake kwa kiasi kikubwa, amesema mafunzo hayo waliyopatiwa yatawasaidia kuwa na uwelewa mpana wa namna ya kusimamia shughuli nzima za lishe katika wilaya zao kwa ufasa.

Mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo wa kutengeneza bajeti za lishe katika mkoa wa Arusha  yaliyosimamiwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) yalifanyika kwa kuhusisha wilaya mbili ya Jiji la Arusha na Arusha Vijiji na kuendelea katika wilaya nyingine za Meru, Longido,Monduli,Karatu na Ngorongoro.


Wednesday, October 24, 2018

MATOKEO YA DARASA LA SABA- 2018

https://www.necta.go.tz/results/2018/psle/psle.htm

Wednesday, October 10, 2018

TAIFA LISILO NA UTAMADUNI NI TAIFA LILILOKUFA

Katibu mkuu wa wizara ya habari,Utamaduni,sanaa na michezo, Suzan Mlawi amesema,Taifa lisilo na utamaduni ni taifa linalokufa na kutoa kizazi kisichoweza kuenzi na kuthamini mila na desturi zao.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua tamasha la Urithi wa Utamaduni katika mkoa wa Arusha lililoanza Octoba 8, 2018 hadi Octoba 13 katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid.

“Nimefarijika kuona tamasha hili litakuwa linafanyika kila mwaka, kwani litatoa nafasi kubwa sana kwa watanzania kujifunza tamaduni mbalimbali na pia litaenzi mila na desturi zetu kwa kiasi kikubwa”,alisema.

Amesema kupitia tamasha hili anategemea kuona ukuaji wa uchumi kwani bidhaa nyingi za asili zitapata masoko,kufufua mila na desturi zilizokufa kwa vijana wa sasa.
 Mwenyekiti wa kamati kuu ya maandalizi  Pro.Audax Mabula, amesema tamasha hili lilizinduliwa mnamo Septemba 15,2018 na makamu wa Rais mheshimiwa Samia Suluhu Hasan mjini Dodoma na kuendelea  Zanzibar, Dar es Salaam na sasa lipo mkoani Arusha.

Amesema lengo kubwa la tamasha hili ni kuenzi mila na malikale za Kitanzania kwani ni kwa mda mrefu sasa  utamaduni wa watalii ndio umekuwa ukipewa kipaombele zaidi kuliko huu utalii wa utamaduni.

Kupitia tamasha hili la urithi wa utamaduni itasaidia kuutambulisha zaidi urithi wa utamaduni katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.

 Nae katibu tawala wa mkoa wa Richard Kwitega amesema tamasha hili kwa mkoa wa Arusha litasaidia kwa kiasi kikubwa kudumisha mila na desturi za makabila ya mkoa huu na pia kuwakutanisha makabila mbalimbali na kuweza kujifunza tamaduni zetu.

Tamasha hili la urithi wa utamaduni lilizinduliwa kwa mala ya kwanza nchini jijini Dodoma na litakuwa likifanyika kila mwaka kwa mwezi mzima wa Septemba katika mikoa mbalimbali na kwa Mkoa wa Arusha linafanyika pia katika wilaya ya Karatu.






Friday, October 5, 2018

UGONJWA WA VIKOPE TISHIO

Viongozi wa Wilaya wa Mkoa wa Arusha wametakiwa kusimamia kikamilifu zoezi la utoaji dawa za ugonjwa wa vikope (Trakoma) kwenye maeneo yao kwa lengo la kuhakikisha ugonjwa huu unatokomezwa kabisa.

Akitoa rai hiyo alipokuwa akifungua semina ya mpango wa kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaombele  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, katibu tawala wa mkoa Richard Kwitega amesema ni vizuri viongozi wakajikita kwa nguvu zote katika zoezi hili lakutokomeza ugonjwa wa vikope kwenye maeneo yao.

“Ni rai yangu kwenu viongozi wote wa Wilaya na halmashauri kuhakikisha mnasimamia vyema zoezi hili lakutokomeza ugonjwa huu wa vikope katika maeneo yenu”.
Lengo la serikali nikutumia rasilimali chache kuthibiti magonjwa haya ambayo yanaonekana hayapewi kipaombele katika jamii yetu hivyo kila halmshauri ihakikishe inatenga fedha zakutosha zakusaidia upasuaji wa vikope.
Wilaya ya Karatu na halmashauri ya Arusha zimejitaidi kuhakikisha zimetokomeza ugonjwa wa vikope lakini bado katika halmashauri ya wilaya ya Longido na Ngorongoro, nguvu zaidi zinaitajika katika maeneo haya.

Kwa mkoa wa Arusha watu takribani 1076 wameshafanyiwa upasuaji wa vikope katika halmshauri zote za wilaya na magonjwa yanayoongoza katika mkoa huu ni ugonjwa wa Kichocho ,Minyoo ya Tumbo na vikope.

Amewataka washiriki wa semina hiyo kuhakikisha kuwa elimu wanayoipata katika mafunzo hayo wakaitumie vizuri katika kutokomeza magonjwa hayo kwenye maeneo yao.
Nae mratibu wa magonjwa yalisiyopewa kipaombele  kutoka Wizara ya Afya, maendeleo ya jamii,jinsia, wazee na watoto Dokta Upendo Mwingira, amesema takribani magonjwa 17 yasiyopewa kipaombele yapo katika bara la Asia, Amerika ya Kusini na Kusini mwa jangwa la Sahara.

Amesema magonjwa mengine ambayo hayapewi kipaombele ni AIDS, TB, Malaria, Kuumwa na nyoka,Matende, Mabusha, Usubi na Ukoma.
Amezitaja athari mbalimbali zinazotokana na magonjwa haya ni kama mgonjwa kupata ulemavu wa mda mrefu, Udumavu kwa watoto,kupunguza uwezo wa kufanya kazi,unyanyapaaji, kansa ya kibofu cha mkojo, upofu na presha ya ini.


Akitoa taarifa fupi ya ugonjwa wa vikope kwa mkoa wa Arusha Dokta Mwanahawa Kombo kutoka hospitali ya Mkoa Mt. Meru, amesema jumla ya wagonjwa 1076 wameshapasuliwa vikope na halmashauri ya Monduli imefanya vizuri katika kukabiliana na ugonjwa huu kati ya halmashauri 2 za Longido na Ngorongoro.
Semina hii hufanyika kila mwaka kwa lengo la kutoa elimu na takwimu sahihi za hali  halisi ya magonjwa yasiyopewa kipaombele nchini.

Semina hii hufanyika kila mwaka kwa lengo la kutoa elimu na takwimu sahihi za hali  halisi ya magonjwa yasiyopewa kipaombele nchini

Friday, September 14, 2018

MILIONI 469 ZATUMIKA KATIKA UJENZI WA KITUO CHA FYA

Jengo la kituo cha afya kata ya Mto wa Mbu wilayani Monduli,kilichojengwa na serikali kwa kushirikiana na nguvu za wananchi.



Milioni 469 zimetumika katika ujenzi wa kituo cha afya Mto wa Mbu wilayani Monduli.

Akisoma taarifa ya mradi huo Mganga mkuu wa kituo cha afya Dr. Emma Agostino Msofe, amesema ujenzi wa kituo hicho ulianza mwaka 2017 baada ya serikali kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 400.

Pia fedha nyingine zimetoka halmashuri kiasi cha shilingi milioni 30 na wananchi  wamechangia milioni 39.

Ujenzi wa kituo hicho cha afya unaendelea na mpaka sasa majengo yaliyojengwa ni  jengo la upasuaji, jengo la wazazi,jingo kufulia,nyumba ya utumishi,vyoo vya nje na matenki ya kuhifadhia maji.

Amesema kituo hicho cha afya kitawasaidia wananchi kupata huduma bora za afya na katika mazingira bora.

Nae kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa ndugu. Charles Francis Kabeho, amesema wananchi wanatakiwa kukitunza kutuo hicho kwa umakini na pia amewataka watumishi watoe huduma bora na kwa weridi kwa wananchi.


Mwengi wa Uhuru ulianza mbio zake mkoani Arusha Mnamo Septamba 12 katika wilaya ya Ngorongoro kisha wilaya ya Karatu na sasa unaendelea katika wilaya ya Monduli.

Kiongozi wa mbio za Kitaifa ndg. Charles Francis Kabeho, akizundua kituo cha afya cha Mto wa Mbu wilayani Monduli.


Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Charles Kabeho ( mwenye sare ya gwanda) akiwa na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Monduli wakitoka kizindua mradi wa kituo cha afya cha mto wa Mbu.


Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Charles Kabeho akikagua mradi wa kuchakata chakula cha mifugo klatika kijiji cha Mungere kata ya  Esilalei wilayani Monduli.


Monday, August 13, 2018

VIJANA SHIRIKINI KATIKA KUJENGA UCHUMI WA VIWANJA

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge, Kazi,Ajira, Vijana na wenye Ulemavu, Antony Mavunde akiteta jambo na mwakilishi Mkazi kutoka UNFPA  Bi.Jaqueline Mahon,katika kilele cha siku ya vijana,Meru Arusha.

Bilioni 15 zitatumika  kukuza ujuzi kwa vijana zaidi ya milioni 4.4 nchini, ili kuwawezesha vijana kuwa na uwezo wa kushiriki shughuli za uchumi wa viwanda.
Yamesemwa hayo na naibu waziri ofisi ya waziri mkuu, sera,bunge,ajira,vijana na wenye ulemavu Mheshimiwa Antony Mavunde,alipokuwa akihutubia vijana katika kilele cha ziku ya vijana kimataifa Mkoani Arusha.
“Vijana mnatakiwa kuwa mstari wa mbele kushiriki katika shughuli za ukuzaji wa uchumi wa viwanda“.
Serikali imeshaweka kipaombele katika kukuza ujuzi kwa vijana ili kuwapa uwezo wakushiriki shughuli mbalimbali za uzalishaji mali na kuwasaidia kukuza uchumi wao.

 Amesema ukosekanaji wa ujuzi ndio changamoto kubwa inayowakabili vijana wengi kwa sasa, kwani tafiti za  mwaka 2014 zinaonesha kuwa 3.5% ya watu wana ujuzi wa juu, 16.6% wana ujuzi wa kati na 76.9 wana ujuzi wa chini kabisa.

Amesema viwango vya kimataifa vinatambua ujuzi katika 12% uwe wa juu,34% wa kati na 54% niwa chini, hivyo nchini yetu bado inakazi kubwa sana katika kuhakikisha tunafikia kiwango hicho cha kimataifa.

Amewasisitizia vijana wote nchini kuakikisha wanatunza afya zao kwani bado kiwango kikubwa cha maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU) kipo kwa vijana.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,amewataka vijana wasikubali kutumika na watu kwa mambo mbalimbali kama yakisiasa, amesema vijana wanatakiwa kuwa makini katika maamuzi wanayoyataka kuyafanya ili waweze kuamua vitu vyenye tija.

Vijana wakiingia katika viwanja vya chuo cha Patandi kwa Maandamano katika kilele cha siku ya vijana duniani,Arusha.

 Gambo amesema mkoa unaendelea kusimamia shughuli na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na serikali ya awamu hii ya tano.
Nae Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro ambae ndie alikuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo ya kilele cha siku ya vijana, amesema wilaya yake imeshatenga ekari 3000 kwenye eneo la Malula kwa ajili ya uwekezaji na vijana ndio watapewa kipaombele cha kupewa maeneo hayo.

Ameishukuru serikali ya Mkoa kwa kuleta maonesha hayo katika wilaya yake na amesema wananchi wa Arumeru wamefurai na wamepata elimu ya kutosha.

Maadhimisho ya siku ya vijana kimataifa yalianzishwa rasmi na umoja wa mataifa kwa lengo la kutoa fursa kwa vijana kujadili maswala mbalimbali yanayowahusu na kuyatafutia majibu na huanzimishwa kila mwaka Agosti 12 ambapo mwaka huu 2018 yameadhimishwa Mkoani Arusha.

Mheshimiwa Antony Mavunde akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya DSW bwana Peter Owaga katika kilele cha siku ya vijana,Arusha.


Friday, August 3, 2018

HUDUMA YA MALIPO KABLA YA MAJI YAZINDULIWA RASMI ARUSHA

Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa (mwenye suruali ya jinsi) akizindua rasmi matumizi ya malipo kala ya maji kwa mkoa wa Arusha katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha (kushoto kwake) ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo na viongozi wengine wa Mkoa na Wilaya..


Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa akiangalia kifaa kitakachotumika kuingiza namba za malipo ya maji.


Prof. Makame Mbarawa akizungumza na viongozi wa Mkoa na Wilaya baada ya  kuzindua rasmi matumizi ya malipo kabla ya maji, katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha.


Hiki ndicho kifaa kitakachotumika kulipia malipo ya maji pamoja na mita ya kusoma spidi ya maji.


Saturday, July 28, 2018

MIRADI MINGI YA MAJI HAINA UHALISIA WA THAMANI

Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji  Mhe. Stella Manyanya (MB), akipanda mtu kama ishara ya uzinduzi wa sherehe za miaka 50 ya bodi ya Wahandisi tangu kuanzishwa, pembeni yake ni viongozi mbalimbali walioshiriki katika kongamano hilo jijini  Arusha.


Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya (MB) amewaagiza mafundi Sanifu kufanya kazi kwa uwaminifu kwa simamia miradi vizuri.
Ameyasema hayo alipofungua kongamano la kuadhimisha miaka 50 ya bodi ya wahandisi nchini katika ukumbi wa Arusha Tekiniko (Arusha Tech), jijini Arusha.
“Miradi mingi ya halmashauri hasa ya maji haina uhalisia wa gharama zake na wasimamizi wakuu ni nyinyi mafundi Sanifu, niwakati sasa umefika mkafanye kazi zenu kwa uwaminifu”.
Aidha, ameiagiza bodi ya mikopo ya elimu ya juu kuhakikisha inatoa mikopo kwa mafundi sanifu ilikuongeza idadi yao kwani kwasasa wapo 927 ni wachache sana kulingana na mahitaji ya nchi.
Serikali inawathamini na kutambua mchango unaotolewa na mafundi sanifu katika kujenga uchumi wa viwanda, hivyo tumuunge mkono rais wetu kwa juhudi zake anazozionyesha.
Mafundi Sanifu,Mchundo na wahandisi ndio watakaoisaidia serikali kufanikisha ujenzi wa viwanda na kuifanya nchi yetu kuingia katika uchumi wa kati wa viwanda.
Bodi ya wahandisi imefanya kongamano lake kwa mala ya kwanza na hii ni moja yakuadhimisha miaka 50 ya bodi hiyo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1968 na maadhimisho yatafanyika Dodoma Septemba 5-7,2018.


Baadhi wa Wahandisi wakimsikilia mgeni rasmi, waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Eng.Stella Manyanya( hayupo pichani) katika  kongamano la miaka 50 ya bodi ya wahandisi,Jijini Arusha.

Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Eng. Stella Manyanya akihutubia katika kongamano la wahandisi lililofanyika jijini Arusha.


Thursday, May 31, 2018

MPINA AFUNGUA MAONESHO YA WIKI YA MAZIWA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhanga Mpina (wa pili kulia) akikata utepe kuzindua wiki ya maziwa Kitaifa kwenye uwanja wa maonyesho ya Kilimo na  Mifugo Nanenane Njiro,kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na viongozi wa Baraza la Kilimo na Bodi ya Maziwa.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Luhanga Mpina akitoa hotuba yake kwenye uzinduzi wa wiki ya Maziwa Kitaifa kwenye uwanja wa maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro jijini Arusha.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi mheshimiwa Luhanga Mpina, ameiagiza bodi ya maziwa kwa kushirikiana na baraza la kilimo Tanzania kuandaa maonyesho ya kimataifa ya wiki ya maziwa badala kila mwaka kuadhimisha yakitaifa tu.
Ameyasema hayo alipokuwa akufungua maonyesho ya 21 ya wiki ya maziwa kitaifa, yaliyofanyika katika viwanja vya Themi Njiro jijini Arusha.
Amewataka kuendelea kusimamia sheria na kanuna za maziwa zinazotumika katika kila nchi, kwani soko la maziwa linapanuka kwa kasi sana.
Aidha, amesisitiza kuwa serikali inaendelea kuhakikisha inabadilisha sheria na kanuni ambazo zinaonekana hazina tija katika sekta hiyo, hii itasaidia sana katika uboreshaji wa soko la maziwa ndani na nje ya nchi.
Amewahasa wafugaji waendelee kutumia ufugaji wa kisasa kwani utaongeza uzalishaji wa maziwa kwa wingi nakutoa fursa zaidi za masoko kwa nchi za nje.
Nae Mkuu wa Mkoa wa Arusha ameipongeza sana bodi ya maziwa kwa kufanikisha madhimisho hayo ya wiki ya maziwa na amewataka wazalishaji wazingatie zaidi sheria na kanuni za ndani na nje ya nchi ili kuepuka usumbufu usiokuwa wa lazima.
Magreti Kihumbuli mwakilishi kutoka bodi ya maziwa Kenya, ameishukuru bodi ya maziwa Tanzania kwa kuwapa mwaliko wakushiriki maonyesho hayo.
Amesema anatagemea kujifunza mambo mengi katika maonyesho hayo na hata pia waonyeshaji wa Tanzania watajifunza mengi kutoka kwao na hii itasaidia kuongeza uhusiano bora kati ya nchi hizi.
Luge Kawaga ni mwakilishi kutoka mamlaka ya endelezaji wa maziwa nchini Uganda, amesema maonyesho hayo yatasaidia kubadilisha elimu baina ya nchi hizo tatu.
Maonyesho ya wiki ya maziwa kitaifa yanafanyika mkoani Arusha kwa siku 3 ambapo makapuni takribani 40 yakiwemo ya kigeni yameweza kushiriki maonyesho hayo.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhanga Mpina akiwapa wanafunzi wa Shule ya Msingi Baraa ya Jijini Arusha baada ya kuzinduawiki ya Maziwa Kitaifa kwenye uwanja maonesho ya Kilimo na Mifugo Nanenane Njiro,kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.


Meneja wa Kampuni ya Milkcom maarufu Dar Fresh,Tunnu Mssika akimpa maelezo Waziri wa Mifugo na Uvuvi wakati akikagua mabanda ya waoneshaji bidhaa mbalimbali zinazotokana na Mifugo.








Wednesday, May 16, 2018

VITUO VYA AFYA KUJENGWA LONGIDO

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa na Mbunge wa jimbo la Longido Dkt. Steven Kiruswa, wakishirikiana na wananchi wa kata ya Ketumbeini kukusanya mawe kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha kata hiyo,wilayani Longido.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema wananchi wa kata ya Kimokouwa na Namanga kwa ujumla hawana haja yakupata matibabu tena kutoka nchi jirani ya Kenya.
Aliyasema hayo alipokagua ujenzi wa kituo cha afya cha Eworendeke katika kata ya Kimokouwa wilayani Longido.
Gambo amesema kwa mda mrefu sana wananchi wa Namanga kwa ujumla walikuwa wanapata hadha yakufuata huduma ya matibabu Longido mjini au nchi jirani ya Kenya na hivyo kufanya wagonjwa wengi kutembea umbali mrefu.
Amesema kituo hicho cha afya kimepata mgao wa shilingi milioni 700 kutoka serikalini na wananchi wanachangia nguvu kazi katika kukijenga na mpaka sasa kiasi cha milioni 400 ndio kimeshatumika na ujenzi unaendelea.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akikagua ujenzi wa kituo cha afya cha Engarenabor kitakacho gharimu kiasi cha milioni 200 mpaka kukamilika.

Gambo amesema mbali na serikali kutoa kiasi hicho cha fedha bado bajeti ya ununuzi wa madawa umeongezwa kutoka bilioni 31 hadi bilioni 269 kwa mwaka huu wa fedha, na hii itasaidia huduma ya madawa kupatikana kiurahisi katika kila kituo cha afya na hospitali zote nchini.
Kituo cha afya cha Eworendeke kinatarajia kukamilika Agosti 2018 na huduma zote zitapatikana zikiwemo huduma za  upasuaji na x-ray, hivyo itarahisisha matibabu kwa wananchi wote wa Namanga.
Mkuu wa Wilaya ya Longido Daniel Chongolo,amesema asilimia 27 ya wajawazito walikuwa wanajifungulia katika vituo vya afya kwa wilaya nzima na idadi imeongezeka kufikia asilimia 35.
Chongolo amesema ongezeko hili litasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto katika wilaya yake.

Ujenzi wa kituo cha afya cha Eworendeke Namanga unaondelea na kituo kitagharimu kiasi cha milioni 700 fedha kutoka serikalini,kituo kipo wilayani Longido.

Mgaga mkuu wa Mkoa Dokta Vivian Wonanji,amesema serikali imeshatenga kiasi cha fedha cha milioni 200 kwa ajili ya manunuzi ya vifaa kwa vituo vyote vya afya na hospitali kwa mkoa mzima na anaendelea na zoezi la kuongeza watumishi katika sekta ya afya.
Amesema agizo la serikali ni kuhakikisha vituo vyote vya afya vinakuwa na huduma ya x-ray, hivyo katika kituo hicho wanajenga chumba maalumu kitakachotoa huduma hiyo kwa wananchi wote wa Namanga.
Akitoa shukurani zake za dhati kwa serikali bwana Hassan Hamis ambae ni mkazi wa Namanga amesema kweli kituo hicho cha afya kitasadia kuondokana na hadha waliyokuwa wanaipata kufuata matibabu kwa umbali mrefu, na pia itapunguza vifo vilivyokuwa vinatokana na umbali huo.
Gambo anaendelea na ziara yake katika wilaya ya Longido ambapo ametembelea kituo kingine cha afya cha  Engarenaibor kilichogharimu kiasi cha milioni 200, pia ameshiriki ujenzi wa kituo cha afya cha kata ya Ketumbeine.

Monday, May 14, 2018

LONGIDO YAPATIWA SIKU 7 KUJIBU HOJA ZA CAG

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo, akisoma baadhi ya hoja zilizotolewa na mkaguzi wa nje (CAG) katika kikao chake na watumishi wa halmashauri ya Longido.

Halmashauri ya Wilaya ya Longido imepewa siku 7 kuhakikisha imejibu hoja zote zilizotolewa na mkaguzi wa nje (CAG) kwa mwaka fedha kuanzia 2015 hadi 2017.
Akitoa agizo hilo mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, amesema halmashauri kupata hati ya mashaka kwa hoja zinazojibika na zinazojirudia kila mwaka ni uzembe wa baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo.
“Watumishi bado wapo wachache wanaofanya kazi  kwa mazoea bila ya kufuata sheria na taratibu za kiutumishi”.
Ameuwagiza uongozi wa halmashauri ya Longido kutoa barua za onyo kwa watumishi wote waliotajwa kwenye taarifa ya mkaguzi wa nje ili iwe fundisho kwa watumishi wote umma.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega,amesema ifike wakati sasa viongozi kutoonea huruma mtumishi yoyote anaebainika ana makosa, kwani hoja nyingi katika halmashuri hiyo zimekuwa zikijirudiarudia kila mwaka.
Amesema  hatua madhubuti ni lazima sasa zichukuliwe ili kudhibiti tabia hii ya mazoea ya hoja kujirudiarudia kila mala.
Akisisitiza zaidi mkuu wa wilaya ya Longido Daniel Chongolo amesema kazi ya viongozi ni kusimamia sheria na taratibu za kazi,hivyo ataendelea kusimamia  sheria za utumishi wa umma katika halmshauri yake kwani mpaka sasa hali imeanza kubadilika kwa watumishi kuwa na nidhani.
Aidha, amesema halmshauri ipo tayari kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na mkuu wa mkoa na kuhakikisha halmashauri yake haitapata tena hati ya mashaka kwa miaka inayokuja.
Gambo yupo katika ziara ya siku 3 wilayani Longido ambapo atatembelea miradi mbalimbali ya maendeleo iliyofanywa katika wilaya hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Longido Daniel Chongolo akimchukuru Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo baada ya kutoa maelekezo ya namna ya kujibu hoja za CAG.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, akizungumza na watumishi wa halmashauri ya Longido alipokuwa akuzungumzia hoja za CAG.