RC Akiapishwa

Dk. John Pombe Magufuli akimuapisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha ,Mhe. Mrisho Gambo.

Ziara ya Waziri Mkuu wa Tanzania

Mhe. Mrisho Gambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa Ofisini kwake, Jijini Arusha.

JPM ,Mrisho Gambo Picha ya Pamoja

Dk. John Pombe Magufuli akipiga picha ya pamoja na mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.

Samia Suluhu Hassan akiwasili Jijini Arusha

Mkuu wa Mkoa Arusha, Mhe Mrisho Gambo Akimpokea Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Picha ya Pamoja

Mhe. Mrisho Gambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa.

Showing posts with label Miundombinu. Show all posts
Showing posts with label Miundombinu. Show all posts

Sunday, December 2, 2018

MAGUFULI NA KENYATA WAFUNGUA KITUO CHA FORODHA CHA PAMOJA


Kituo cha forodha cha mpaka wa Namanga mkoani Arusha kinatarajia kukusanya mapato ya kiasi cha bilioni 53 kwa mwaka 2019.

Yamesemwa hayo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akifungua kituo cha pamoja cha forodha kati ya Tanzania na Kenya katika mpaka wa Namanga Arusha.

“Vituo hivi vya huduma ya pamoja vinasaidia kurahisisha usafiri, kukuza biashara na utalii na urahisi kwa wananchi wetu kuvuka mpakani mara  kwa mara.”

Amesema nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinachangamoto ya kuwa na vikwanzo vya kibiashara vinavyopeleka uchumi wa nchi hizi kudolola ukilinganisha na mabara mengine kama ya Amerika.

Kutokana na changamto hiyo nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zikachukua uwamuzi wa kuanzisha vituo vya forodha vitakavyo saidia kukuza biashara kwa nchi husika.

Nae Rais wa Jamhuri ya Kenya Uhuru Kenyata amesema, kituo hicho kiwe chachu ya kuwasaidia wafanyabiashara wadogo kukuza biashara zao kwani wao ndio msingi wa uchumi katika nchi zetu.
Kenyata amesema ni wajibu wa watumishi wa kituo hicho kuwasaidia na kuwajali wafanyabiashara hao wadogo na wao wafanyabiashara wafuate sheria za nchi husika na biashara zao ziwe halali.

Amesema jukumu la serikali ni kuhakikisha wananchi wake wanafanya biashara kwa haki na uhuru bila ubuguzi wowote.

Gavana wa jimbo la Kajado Joseph Oleleku, alisema ili nchi hizi mbili ziweze kunufaika na fursa za biashara amekuwa akifanya mikutano ya mara kwa mara ili kuhakikisha wafanyabaishara wanapata haki zao na wanafanya biashara zao kwa uhuru.

Akitoa neno la ukaribisho mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema,Mkoa umeendelea kuhakikisha usalama wa mpaka huo unaimarika kwa kiasi kikubwa kwa kuongeza ulinzi wa kutumia mbwa.

Gambo amesema mbali na huduma nzuri iliyopo katika mpaka huo kuna changamoto ya ukosefu wa scanna kwa ajili ya ukaguzi wa magari makubwa, ukosefu wa huduma ya upimaji wa ubora wa bidhaa  zinazoingia na kutoka mpakani.

Magufuli yupo katika ziara ya siku 2 mkoani Arusha ambapo amefungua kituo cha pamoja cha forodha na ataweka jiwe la msingi katika mradi mkubwa wa maji katika jiji la Arusha na wilaya ya Arumeru.

Friday, November 23, 2018

TUNZENI VYANZO VYA MAJI

 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, imeiagiza bodi ya Mamlaka ya maji safi na Usafishaji Mazingira ya jiji la Arusha AUWSA kuweka kipaombele katika utunzaji wa vyanzo vya maji viliyopo katika mlima Meru.

Ameyasema hayo alipokuwa  katika ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya maji katika jiji la Arusha.

“Nimewahi kusikia wataalam wa maji wakisema Vita ya Tatu ya dunia itahusisha kugombea maji,ninaomba sisi tuanze kujihami kwa kutunza vyanzo vyetu vya maji.Niitake bodi ya AUWSA kuandika andiko la mradi ambalo tutalipigia debe katika ofisi ya Makamu wa Rais inayoshughulikia Mazingira ili kuweza kupata ufadhili wa kampeni yetu hii ya utunzaji wa vyanzo vya maji”.

Gambo alisema,itakuwa haina maana kutumia kiasi kikubwa cha fedha za serikali katika uboreshaji wa huduma za maji na baada ya miaka michache ijayo vyanzo vyote vikauke.
 Nae Mkurugenzi wa Mmlaka ya Maji safi na usafirishaji (AUWSA) Mhandisi Ruth Koya amesema, mradi huo utakamilika June 2020 na Arusha itanufaika sana na mradi huo kwakuwa  ukosefu wa maji utakuwa historia.

Amesema tayari wakandarasi wameshaanza kusambaza mtandao wa maji safi na taka kwa kuweka mabomba ya kisasa yanayoendana na mahitaji ya sasa.

Aidha, amesema mpaka mradi huu ukamilike upatikanaji wa maji katika jiji la Arusha utafikia asilimia 100 tofauti na hali ya sasa ambapo ni asilimia 44 tu ya wananchi ndio wanapata maji safi.
 Ruth alisema, uzalishaji wa maji utaongezeka kutoka wastani wa lita milioni 40 hadi lita milioni 200 kwa siku na upotevu wa maji utashuka toka asilimia 40 za sasa hadi wastani wa asilimia  25.

Mwenyekiti wa bodi ya AUWSA, Dk. Richard Masika ameipongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuweza kutoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 520 kupitia mkopo wa riba nafuu kutoka benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika kufanikisha mradi huu mkubwa na ametoa rai kwa wananchi wa Arusha kuitunza muindombinu iliyopita katika maeneo yao kwa ajili ya manufaa ya leo na baadae.

Gambo yupo katika ziara ya siku 3 katika wilaya ya Arusha, Arumeru na Longido akikagua miradi ya maji inayoendeleo katika maeneo hayo.


Friday, September 14, 2018

MILIONI 469 ZATUMIKA KATIKA UJENZI WA KITUO CHA FYA

Jengo la kituo cha afya kata ya Mto wa Mbu wilayani Monduli,kilichojengwa na serikali kwa kushirikiana na nguvu za wananchi.



Milioni 469 zimetumika katika ujenzi wa kituo cha afya Mto wa Mbu wilayani Monduli.

Akisoma taarifa ya mradi huo Mganga mkuu wa kituo cha afya Dr. Emma Agostino Msofe, amesema ujenzi wa kituo hicho ulianza mwaka 2017 baada ya serikali kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 400.

Pia fedha nyingine zimetoka halmashuri kiasi cha shilingi milioni 30 na wananchi  wamechangia milioni 39.

Ujenzi wa kituo hicho cha afya unaendelea na mpaka sasa majengo yaliyojengwa ni  jengo la upasuaji, jengo la wazazi,jingo kufulia,nyumba ya utumishi,vyoo vya nje na matenki ya kuhifadhia maji.

Amesema kituo hicho cha afya kitawasaidia wananchi kupata huduma bora za afya na katika mazingira bora.

Nae kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa ndugu. Charles Francis Kabeho, amesema wananchi wanatakiwa kukitunza kutuo hicho kwa umakini na pia amewataka watumishi watoe huduma bora na kwa weridi kwa wananchi.


Mwengi wa Uhuru ulianza mbio zake mkoani Arusha Mnamo Septamba 12 katika wilaya ya Ngorongoro kisha wilaya ya Karatu na sasa unaendelea katika wilaya ya Monduli.

Kiongozi wa mbio za Kitaifa ndg. Charles Francis Kabeho, akizundua kituo cha afya cha Mto wa Mbu wilayani Monduli.


Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Charles Kabeho ( mwenye sare ya gwanda) akiwa na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Monduli wakitoka kizindua mradi wa kituo cha afya cha mto wa Mbu.


Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Charles Kabeho akikagua mradi wa kuchakata chakula cha mifugo klatika kijiji cha Mungere kata ya  Esilalei wilayani Monduli.


Saturday, July 28, 2018

MIRADI MINGI YA MAJI HAINA UHALISIA WA THAMANI

Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji  Mhe. Stella Manyanya (MB), akipanda mtu kama ishara ya uzinduzi wa sherehe za miaka 50 ya bodi ya Wahandisi tangu kuanzishwa, pembeni yake ni viongozi mbalimbali walioshiriki katika kongamano hilo jijini  Arusha.


Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya (MB) amewaagiza mafundi Sanifu kufanya kazi kwa uwaminifu kwa simamia miradi vizuri.
Ameyasema hayo alipofungua kongamano la kuadhimisha miaka 50 ya bodi ya wahandisi nchini katika ukumbi wa Arusha Tekiniko (Arusha Tech), jijini Arusha.
“Miradi mingi ya halmashauri hasa ya maji haina uhalisia wa gharama zake na wasimamizi wakuu ni nyinyi mafundi Sanifu, niwakati sasa umefika mkafanye kazi zenu kwa uwaminifu”.
Aidha, ameiagiza bodi ya mikopo ya elimu ya juu kuhakikisha inatoa mikopo kwa mafundi sanifu ilikuongeza idadi yao kwani kwasasa wapo 927 ni wachache sana kulingana na mahitaji ya nchi.
Serikali inawathamini na kutambua mchango unaotolewa na mafundi sanifu katika kujenga uchumi wa viwanda, hivyo tumuunge mkono rais wetu kwa juhudi zake anazozionyesha.
Mafundi Sanifu,Mchundo na wahandisi ndio watakaoisaidia serikali kufanikisha ujenzi wa viwanda na kuifanya nchi yetu kuingia katika uchumi wa kati wa viwanda.
Bodi ya wahandisi imefanya kongamano lake kwa mala ya kwanza na hii ni moja yakuadhimisha miaka 50 ya bodi hiyo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1968 na maadhimisho yatafanyika Dodoma Septemba 5-7,2018.


Baadhi wa Wahandisi wakimsikilia mgeni rasmi, waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Eng.Stella Manyanya( hayupo pichani) katika  kongamano la miaka 50 ya bodi ya wahandisi,Jijini Arusha.

Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Eng. Stella Manyanya akihutubia katika kongamano la wahandisi lililofanyika jijini Arusha.


Wednesday, May 16, 2018

VITUO VYA AFYA KUJENGWA LONGIDO

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa na Mbunge wa jimbo la Longido Dkt. Steven Kiruswa, wakishirikiana na wananchi wa kata ya Ketumbeini kukusanya mawe kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha kata hiyo,wilayani Longido.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema wananchi wa kata ya Kimokouwa na Namanga kwa ujumla hawana haja yakupata matibabu tena kutoka nchi jirani ya Kenya.
Aliyasema hayo alipokagua ujenzi wa kituo cha afya cha Eworendeke katika kata ya Kimokouwa wilayani Longido.
Gambo amesema kwa mda mrefu sana wananchi wa Namanga kwa ujumla walikuwa wanapata hadha yakufuata huduma ya matibabu Longido mjini au nchi jirani ya Kenya na hivyo kufanya wagonjwa wengi kutembea umbali mrefu.
Amesema kituo hicho cha afya kimepata mgao wa shilingi milioni 700 kutoka serikalini na wananchi wanachangia nguvu kazi katika kukijenga na mpaka sasa kiasi cha milioni 400 ndio kimeshatumika na ujenzi unaendelea.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akikagua ujenzi wa kituo cha afya cha Engarenabor kitakacho gharimu kiasi cha milioni 200 mpaka kukamilika.

Gambo amesema mbali na serikali kutoa kiasi hicho cha fedha bado bajeti ya ununuzi wa madawa umeongezwa kutoka bilioni 31 hadi bilioni 269 kwa mwaka huu wa fedha, na hii itasaidia huduma ya madawa kupatikana kiurahisi katika kila kituo cha afya na hospitali zote nchini.
Kituo cha afya cha Eworendeke kinatarajia kukamilika Agosti 2018 na huduma zote zitapatikana zikiwemo huduma za  upasuaji na x-ray, hivyo itarahisisha matibabu kwa wananchi wote wa Namanga.
Mkuu wa Wilaya ya Longido Daniel Chongolo,amesema asilimia 27 ya wajawazito walikuwa wanajifungulia katika vituo vya afya kwa wilaya nzima na idadi imeongezeka kufikia asilimia 35.
Chongolo amesema ongezeko hili litasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto katika wilaya yake.

Ujenzi wa kituo cha afya cha Eworendeke Namanga unaondelea na kituo kitagharimu kiasi cha milioni 700 fedha kutoka serikalini,kituo kipo wilayani Longido.

Mgaga mkuu wa Mkoa Dokta Vivian Wonanji,amesema serikali imeshatenga kiasi cha fedha cha milioni 200 kwa ajili ya manunuzi ya vifaa kwa vituo vyote vya afya na hospitali kwa mkoa mzima na anaendelea na zoezi la kuongeza watumishi katika sekta ya afya.
Amesema agizo la serikali ni kuhakikisha vituo vyote vya afya vinakuwa na huduma ya x-ray, hivyo katika kituo hicho wanajenga chumba maalumu kitakachotoa huduma hiyo kwa wananchi wote wa Namanga.
Akitoa shukurani zake za dhati kwa serikali bwana Hassan Hamis ambae ni mkazi wa Namanga amesema kweli kituo hicho cha afya kitasadia kuondokana na hadha waliyokuwa wanaipata kufuata matibabu kwa umbali mrefu, na pia itapunguza vifo vilivyokuwa vinatokana na umbali huo.
Gambo anaendelea na ziara yake katika wilaya ya Longido ambapo ametembelea kituo kingine cha afya cha  Engarenaibor kilichogharimu kiasi cha milioni 200, pia ameshiriki ujenzi wa kituo cha afya cha kata ya Ketumbeine.

Friday, April 27, 2018

KATIBU TAWALA AKUTANA NA WAJUMBE KUTOKA BENKI YA DUNIA

Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Richard Kwitega, akiwa na wajumbe kutoka Benki ya Dunia ofisini kwake pamoja na wataalamu kutoka katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Arusha.


Kiongozi wa ujumbe kutoka Benki ya Dunia Bwana Nicholas Soikan (mwenye suti ya blue) akiandika maelezo yaliyokuwa yanatolewa na wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa (Hawapo pichani),katika ofisi ya katibu tawala,Arusha.


Katibu Tawala Bwana Richard Kwitega,akiongoza kikao kilichowakutanisha ujumbe kutoka Benki ya Dunia na wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Arusha.



Friday, May 5, 2017

RC GAMBO AFUNGUA SEMINA ELEKEZI KWA VIONGOZI WA MKOA.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha mrisho Gambo pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro wakisiliza mafunzo elekezi ya viongozi wa mkoa wa Arusha.     


Viongozi wa Mkoa wa Arusha wameshauriwa kuwajibika katika majukumu yao huku wakifuata kanuni na sheria mbalimbali za utumishi wa umma ili kuongeza ufanisi katika maeneo yao ya kazi huku wakileta maendeleo kwa mkoa.

Akifungua mafunzo elekezi kwa viongozi hao  Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema viongozi wa mkoa wa Arusha wanatakiwa kuongeze mahusiano katika maeneo yao ya kazi baina yao na watumishi wachini yao.

Amesema lengo kubwa nikuondoa migongano inayojitokeza baina ya viongozi na watumishi hao ambayo inapelekea kudhorotesha utendaji  wa kazi katika maeneo yao na kuongezeka wimbi la uwonevu kwa watumishi wao.

Aidha amewataka viongozi hao wasimamie uwajibikaji wa watumishi katika maeneo ya kazi kwa kufuata taratibu za majukumu yao.

Akisisitiza zaidi kwa kuwataka viongozi kutekeleza maelekezo yanayotolewa na ngazi za juu serikalini kwani mengi yanakuwa ni miongoni mwa shughuli zao za kila siku na hii itaongeza utii kwa viongozi serikalini.

Nae katibu tawala wa mkoa  Richard  Kwitega amesema mafunzo hayo niyakukumbushana majukumu kwa viongozi hao huku wakipitia maeneo mbalimbali ikiwemo wajibu na majukumu ya viongozi,usimamizi wa Rasilimali watu sehemu za kazi napia kupitia kanuni na maadili ya viongozi na utumishi wa umma.

Amesema mafunzo hayo yatakuwa ya siku 2 huku yakishirikisha baadhi ya viongozi kutoka TAMISEMI.

Mkuu  wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro na Mkuu wa Wilaya ya Monduli Idd Kimanta wakisikiliza mafunzo ya viongozi wa Mkoa wa Arusha yaliyotolewa kwa lengo lakukuza uwelewa.

Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Arusha waliohudhuria mafunzo elekezi kwa viongozi wa mkoa wa Arusha.

WAZIRI MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA TENGERU SAKINA

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa akitoa malekezo kwa viongozi wa mkoa wa Arusha alipokuwa akikagua barabara inayojengwa ya Tengeru  mpaka Sakina, jijini Arusha.

Mhe.Kassim Majaliwa akiwa pamoja na viongozi wa Mkoa wakikagua barabara inayojengwa ya Tengeru mpaka Sakina,Jijini Arusha.

Saturday, March 25, 2017

Wanawake wapigwa marufuku kushinikizwa kuandamana.

Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Loliondo wakiandamana kupinga kamati wa utatuzi wa mgogoro wa pori tengefu.


BAADHI ya Wanawake  pamoja na watoto  wanatumiwa kama chambo  kwaajili ya  kusimamisha msafara wa Kamati ya Kukamilisha mchakato wa Utatuzi wa  Mgogoro wa Matumizi ya Ardhi kwenye Pori Tengefu la Loliondo.

Kutumika kwa wanawake hao ambao baadhi yao walikuwa na watoto wadogo migongoni kumebainika jana wakati kamati hiyo ilipokuwa ikiendelea kuangalia maeneo mbalimbali ya Pori hilo Tengefu la Loliondo lenye ukubwa wa kilomita 15,000 za mraba zilizoleta mgogoro kwa zaidi ya miaka 25 sasa.

Wanawake hao katika Kata ya Malambo na Kata ya  Arash,ambao kwa pamoja walibeba mabango  ya kuisihi Kamati hiyo kutenda haki mengine
yakimtuhumu Waziri wa Maliaisili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe
wakidai kuwapenda wanyamapori kuliko binadamu.


Baadhi ya wanwake hao ambao ni  Rehema Pascal na Lemnyaki John
walisimamisha mafara huo kwakuonyesha mabango yao yanayodai kutokubali kuhamishwa katika Pori hilo huku wengine wakipandisha mori na kupiga mayowe.


Baada ya Rc,Gambo kuyasoma mabango hayo aliwapa vipaza sauti ili
wayasome tena hapo ndipo waliposhindwa kuyasoma na kudai kuwa hawajui Kiswahili.
“Nani aliyewaandikia mabango haya wakati hamjui kusoma ,mnatumiwa na
viongozi wenu hukusu mgogoro huu ,msikubali kutumika maana hamjui
serikali inafanya hivi kwa nia ipi na wala serikali haina mpango wa
kuchukua ardhi hii bali tunachokifanya ni kujua hayo mnayoyasema yapo
kiuhalisia au la ili tukamilishe kazi yetu”.
Naye Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Felex Wandwe alisisitiza
aliwatoa hofu wananchi wa Kata saba za wilaya hiyo kutokubali kutumika
vibaya kwaajili ya Pori hilo kwani serikali inachofanya hivi sasa ni
kuchukua mapendekezo ya kamati hiyo kisha kuyawasilisha kwa Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa .


“Msikubali kutumiwa kwa maslahi ya wengine sisi tupo pamoja na
wawakilishi wenu na kabla ya kuanza zoezi hili walijua tunakuja
kufanya nini hivyo mtulie”.
Pia Katibu wa Kamati hiyo, Bahati Chisanza alisema kuwa ni vyema
wananchi wakajua kuwa serikali haichukui ardhi bali inachokifanya ni
kutaka kupanga matumzii bora ya ardhi ili kila mtu anufaike nayo.


Awali Mwenyekiti wa Kijiji cha  Malambo, Lazaro Mashele alitoa rai kwa
kamati hiyo kutoiingiza Kata hiyo ya Malambo katika matumizi bora ya
ardhi kwani kata hiyo haina mgogoro na Pori hilo bali ni wahifadhi
wazuri wa wanyamapori ingawa kata hiyo ni sehemu ya mazalia ya
wanyama.


“Tunawaomba wakuu kata hii isiingizwe katika  mgogoro huu kwani hatupo
ndani ya vijiji saba lakini pia kata hii inatumika kwaajili ya mazalia
ya wanyamapori ambao hatuna ugomvi nao”.


Aidha  Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gambo alisisitiza kuwa wamechukua maoni ya mwenyekiti huyo na watafanyia kazi maoni yote yaliyotolewa na
wananchi hao ,wahifadhi na wataalam wa ardhi kisha kuyawasilisha kwa
Waziri Mkuu Machi 25 mwaka huu.


Wakati huo huo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo
alitoa rai kwa wananchi hao  kutokubali kutumika kwa msalahi ya
wengine na kutoa rai kwa viongozi wa vijiji,madiwani na mashirika
yasiyo ya kiserikali kuacha mara moja kuwatumia wananchi kwaajili ya
kuwapotosha kuhusu Pori Tengefu la Loliondo.


Pia alisema polisi wataanza msako kwa wale wote ambao si raia wa
Tanzania wanaoishi Wilayani Loliondo huku akisisitiza kuwa wamemkamata
mtu mmoja ambaye ni mwanaume (hakumtaja jina) kwa kufanya vurugu
wakati kamati hiyo ilipokuwa ikifanya kazi yake katika kata mbalimbali
na muda wowote atafikishwa mahakamani wilayani humo.



Thursday, November 24, 2016

ZAIRA YA SAMIA SULUHU HASSANI KATIKA KIWANDA CHA MT,MERU MILLERS

Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo ya malighafi inayotumika katika kutengenezea mafuta yatokanayo na alizeti katika kiwanda cha Mt. Meru Millers, jijini Arusha.

Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassani ametembelea kiwanda cha Mt. Meru Millers Limited  cha jijini Arusha kinachojishughulisha na utengenezaji wa mafuta yatokanayo na alizeti.

Akizungumza baada yakujionea uzalishaji wakiwanda hicho,amesema lengo kubwa ya ziara yake katika kiwanda hicho ilikuwa nikujionea shughuli zinazofanywa na kiwanda hicho.

Pia ameweza kusikiliza changamoto mbalimbali zinazozikabili kiwanda hicho na kubwa ikiwa ni utozwaji wa kadi nyingi na serikali itahakikisha kunakuwa na utaratibu mzuri wa ulipaji wa kodi hizo.

Aidha alisisitiza zaidi kuwa serikali ya awamu wa tano imedhamilia ujenzi wa viwanda vingi nchini ambavyo vitatumia malighafi za ndani ya nchi nakukuza uzalisha kwa wakulima na hata pia kutoa ajira za kutosha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mt. Meru Millers Atul Mittal alisema ikiwa serikali itapunguza kodi hizi nyingi itasaidia ukuwaji wa viwanda vilivyopo na hata kuhamasisha wawekezaji wengine kuwekeza kwenye viwanda hapa nchini.

Makamu wa Rais yupo Mkoa Arusha kikazi kwa mda wa siku 3 ambapo atendelea kutembelea viwanda vya mkoani  hapa na pia atazindua jengo la Mahakama ya Afrika.
Makamu wa Rais,Samia Suhulu Hassan akiangalia moja ya kifungashio cha mafuta ya alizeti kilichotengenezwa na kiwanda cha Mt,Meru Millers,Arusha.

Makamu wa Rais,Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa na wafanyakazi wa kiwanda cha Mt.Meru Millers,jijini Arusha.

Wednesday, November 16, 2016

CHAMA CHA WAMILIKI WA MAGARI YA NOAH WAKABIDHI SIMENTI MIFUKO 200

Mkuu wa Mkoa, Mrisho Gambo akipokea mifuko 200 ya simenti kutoka kwa chama cha wa wamiliki wa magari aina ya Noah cha Jijini Arusha.

Mkuu wa Mkoa, Mrisho Gambo akipokea mifuko 200 ya simenti kutoka kwa chama cha wa wamiliki wa magari aina ya Noah cha Jijini Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo akimkabidhi mifuko 50 ya simenti Mkuu wa Wilaya ya Longido Daniel Chongolo kwaajili ya ujenzi wa kitua cha afya Namanga, Wilayani Longido.

Saturday, October 22, 2016

KAMPUNI YA UKANDARASI KUTOKA KOREA YATOA MSAADA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Mashaka Gambo amepokea mifuko 500 ya simenti na mabati 500 kutoka kwa kampuni ya ukandarasi ya Hanil JV Jiangsu kutoka Korea inayojenga barabara ya Tengeru Sakina.
Msaada huo umetolewa ofisini kwake ambapo tukio hilo limeweza kushuhudiwa na viongozi mbalimbali wa Mkoa,Wilaya na Wabunge wa viti maalumu wa Mkoa wa Arusha.
Akipokea msaada huo,Mrisho Gambo amesema atagawa mifuko 100 ya simenti na mabati 100 kwaajili ya ujenzi wa Zahanati kata ya Murieti kwasababu kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wagonjwa katika hospitali ya Mkoa Mt.Meru wanaotoka maeneo hayo hivyo ujenzi huo utasaidia  kupunguza wagonjwa katika hospitali hiyo.
Pia yatakayo baki atayapeleka Wilaya ya Longido katika kusaidia ujenzi wa bweni la shule ya sekondari Longido ambayo liliungua moto nakuteketeza kila kitu.
“Napenda kuishukuru na kuipotengeza kampuni ya ukandarasi ya barabara ya Tengure Sakina na ile ya njia mbadala(by path) kwakutoa msaada huu na kwakuwa tumeshaanza  mkakati wa ujenzi wa madara kwa shule za msingi na Sekondari,hivyo nitagawa hayo mifuko ya simenti 100 na mabati 100 ikajenge Zahanati kata ya Murieti na yaliyobaki yataenda Longido katika ujenzi wa bweni lililoungua”.
Mkurugenzi  Mtendaji wa kampuni ya ukandarasi ya Hanil JV Jiangsu bwana Xie Jianbao amesema kampuni yao imetoa msaada huo ikiwa ni moja ya shughuli zao zakusaidia jamii katika shughuli mbalimbali za maendeleo.
“Tumetoa mifuko ya simenti 500 na mabati 500 kama moja ya mchango wetu katika kusaidia jamii yetu kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo”.
Aidha Mkurungezi wa Jiji la Arusha,Athumani Kihamia alisema  kutokana na wingi wa wananchi waliopo katika kata ya Murieti Zahanati hiyo itaenda kuwasaidia sana na kwakipindi kisichozidi miezi 2 Zahanati hiyo itakamilika na wananchi wataweza kuitumia.
Ukosefu wa kituo cha afya katika kata ya Muriet ulibainika baada ya Mkuu wa Mkoa Gambo kufanya ziara katika kata hiyo nakupata malalamiko kutoka kwa wananchi kuwa wanatembe umbali mrefu sana kutafuata huduma za afya.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akitoa shukrani kwa kampuni ya ukandarasi ya Hanil JV Jiangsu kwa kutoa msaada wa mifuko ya simenti 500 na mabati ya 500 kwa shughuli za maendeleo za Mkoa wa Arusha.